Mfanyabiashara Dar akamatwa na askari wa uhamiaji


Mfanyabiashara Davis Mosha anashikiliwa na Idara ya Uhamiaji baada ya jana Agosti Mosi, 2018 kukamatwa kwa madai ya kuwazuia askari wa Idara hiyo  kutekeleza majukumu yao

Akizungumza msemaji wa idara hiyo, Ali Mtanda amesema Mosha aliwashambulia askari hao na kumnyang’anya mmoja wao simu ya mkononi baada ya kufika katika jengo la Delina lililopo Sinza Mori, jijini hapa

"Askari walifika kwenye majengo hayo na kujitambulisha kwa mlinzi na moja kwa moja walionyeshwa ofisi za meneja,” amesema Mtanda
“Wakati wakifanya mazungumzo ya kikazi na meneja huyo, ghafla akatokea Mosha na kuanza kuwafokea, kisha kuwashambulia na kumnyang'anya askari mmoja simu yake.”

Amesema alichofanya Mosha ni kinyume cha sheria ya uhamiaji namba 54 kifungu cha 45 kipengele 1 F, kinachozungumzia kumzuia ofisa wa uhamiaji kufanya kazi yake ya ukaguzi

Mtanda amesema bado wanamshikilia Mosha kwa uchunguzi zaidi na kama kuna hatua nyingine zitafuata watatoa taarifa

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jumanne Murilo amesema tayari  wamepokea taarifa ya tukio hilo, wanafanya uchunguzi kwa hatua za kisheria

"Tunachunguza ili kujua kilichotokea ni nini, baada ya hapo ndio hatua nyingine zitafuata,” amesema Murilo
Mfanyabiashara Dar akamatwa na askari wa uhamiaji Mfanyabiashara Dar akamatwa na askari wa uhamiaji Reviewed by KUSAGANEWS on August 02, 2018 Rating: 5

No comments: