Mwanafunzi apandishwa kizimbani akidaiwa kuiba bodaboda

Watu wawili akiwamo mwanafunzi wa Sekondari ya Mugumu Kurwa Daniel (19) na raia wa kawaida Paulo Marwa (30) wamefikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Serengeti mkoa Mara wakidaiwa kuiba pikipiki

Mwendesha mashtaka wa Polisi Renatus Zakeo ameiambia mahakama kuwa washitakiwa hao walitenda kosa hilo Julai 27 mwaka huu

Alikuwa akiwasomea mashtaka hayo leo Agosti 2 mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo Ismail Ngaile

Mwanafunzi Daniel yeye alikamatwa leo Agosti 2 akiwa shule, akasomewa mashtaka akiwa amevaa sare zake za shule na mkononi akiwa meshika madaftari yake

Amesema waliiba pikipiki aina ya Toyo mali ya Benjamin Kiboge yenye thamani ya Sh2 milioni

Washtakiwa wote wamekana mashitaka na wamepelekwa mahabusu hadi Agosti 10 mwaka huu itakapotajwa tena

Mwanafunzi apandishwa kizimbani akidaiwa kuiba bodaboda Mwanafunzi apandishwa kizimbani akidaiwa kuiba bodaboda Reviewed by KUSAGANEWS on August 02, 2018 Rating: 5

No comments: