Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison
Mwakyembe ameitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kutoa mwongozo
utakaowezesha kampuni za ving'amuzi za Azam, DSTV na Zuku kurusha maudhui
ya chaneli za ndani
Amesema kampuni hizo zimelazimika kuondoa chaneli za ndani
katika ving'amuzi vyake baada ya kukiuka masharti ya leseni zao
Dk Mwakyembe ametoa kauli hiyo leo Agosti 14 wakati
akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara Habari Maelezo, jijini Dar es
Salaam.
Amesema kampuni zilipewa leseni ya kuonyesha chaneli za
kulipia lakini zikaingilia soko la wenzao kinyume cha utaratibu wa leseni zao
"Inaelekea hawa wenzetu wanapenda kurusha haya maudhui
ya chaneli za ndani, hivyo TCRA itoe mwongozo wa nini wafanye ili
kuendelea kutoa huduma,” amesema
"Kama wamevutiwa na soko la kurusha maudhui haya basi
wasifanye mbinu za chini chini badala yake wafuate utaratibu," amesema Dk
Mwakyembe
Dk Mwakyembe amesisitiza kuwa kampuni hizo zilivunja
masharti ya leseni zao lakini Serikali iliwavumilia kwa kuheshimu utawala wa
sheria
Mwakyembe aitaka TCRA kutoa mwongozo wa ving’amuzi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 14, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment