Bilioni 476 kuwaondolea Wananchi Kero ya Maji Jiji la Arusha


Kutokana na Tatizo la kero ya upungufu wa majisafi na uondoaji wa majitaka katika jiji la Arusha na baadhi ya maeneo ya wilaya ya Arumeru Serikali imeingia mkataba na kampuni ya Beijin Contuction Engineering Group kwa ajili ya Kuondoa tatizo hilo.

Mkataba huo Leo tar 14 August 2018 umesainiwa na Mkurugenzi wa maji na Usafi wa mazingira AUWSA Bi Ruth Koya pamoja na Kampuni ya Beijin Constuctioni Mbele ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa ambapo ni kuhakikisha wanawaondolea wananchi adha hiyo inayowakabili.

Akizungumza Mkurugenzi wa AUWSA Bi Ruth Koya amesema mradi huo utagharimu fedha za Kitanzania Bilioni 476 na kati ya fedha hizo Sh Bilioni 429 ni mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Maendeleo afrika AfDB ambapo Bilioni 47 ni mchango wa Serikali.

Amesema Lengo la mkataba huo ni kuongeza huduma ya uondoaji wa majitaka kutoka asilimia 7.66 ya jiji la Arusha hadi kufikia asilimia 30 na wananchi 4500 wataunganishwa kwenye mfumo wa uondoaji wa majitaka ambapo jumla ya Bomba zenye km 176.5 zitatumika.

Kwa upande wa Waziri wa maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa amesema mradi huo unatakiwa kutekelezwa ndani ya miaka miwili kuanzia 14 Agost 2018 na kukamilika 13 Agost 2020 na muda wa miezi 12 kwa ajili ya matazamio.

Hata hivyo ametoa rai kwa mkandarasi wa kampuni hiyo ya Beijin Construction kuhakikisha kazi hiyo inakamilika kwa wakati na inatakiwa ifanyike usiku na mchana kwa kuwa tayari fedha zipo kwa ajili ya mradi huo

Amesisitiza kuwa serikali kufanya hivyo ni kwa ajili ya kuboresha hali ya upatikanaji wa majisafi na kuboresha Huduma ya uondoaji wa maji taka katika jiji la Arusha ili kuboresha afya ya hali ya maisha yaw a kazi wa jiji la Arusha na kwa ujumla wake.




Bilioni 476 kuwaondolea Wananchi Kero ya Maji Jiji la Arusha Bilioni 476  kuwaondolea Wananchi Kero ya Maji Jiji la Arusha Reviewed by KUSAGANEWS on August 14, 2018 Rating: 5

No comments: