Mkuu wa Polisi nchini (IGP), Simon Sirro amefanya mabadiliko
madogo kwenye jeshi hilo na kumuondoa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza
(DCP) Ahmed Msangi na kumhamishia makao makuu ya jeshi hilo
Taarifa iliyotolewa leo, Jumatano Agosti 15, 2018 na Msemaji
wa polisi, Barnabas Mwakalukwa imeeleza kuwa Msangi amehamishiwa makao na kuwa
Mkuu wa kitengo cha makosa dhidi ya binadamu makao ya upelelezi Dar es Salaam
Mwakalukwa amesema nafasi ya Msangi imechukuliwa na Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jonathan Shana
“Nafasi wa Shana imechukuliwa na Kamanda Wankyo Nyigesa
aliyekuwa mkuu wa operesheni kanda maalumu ya Dar es Salaam,” amesema
Mwakalukwa
Kwa mujibu wa Mwakalukwa mabadiliko ya uhamisho huo ni ya
kawaida yanatokea ndani jeshi la polisi katika kuongeza ufanisi kwenye utendaji
kazi
IGP afanya mabadiliko Jeshi la Polisi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 15, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment