Mtandao walaani kukamatwa kwa Wakili Arusha


Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), wamelaani kitendo cha kushikiliwa kwa Wakili Mendrad D'Souza pamoja na wateja wake kwa amri ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti na kudai hiyo ni sawa na kuzuia mahakama isifanye kazi yake

Wakili huyo maarufu wa kujitegemea jijini Arusha na wafanyakazi wanne wa kampuni ya wakala wa pembejeo za kilimo Balton Ltd walikamatwa  Julai 30 na kulazwa mahabusu kwa saa 48  na waliachiwa jana jioni. 

Akizungumza na waandushi wa habari leo Agosti Mosi, Mratibu wa mitandao huo, Onesmo Olengurumwa amesema THRDC wanatambua mawakili wanafanya kazi zao za utetezi kwa mujibu wa sheria zilizowekwa na nchi

Hivyo wanastahili kupewa ulinzi na uhuru wa kufanya kazi zao pasipo kuingiliwa na mamlaka za serikali ili waweze kusaidia kutoa haki
"Mtandao unaona kwamba madhara ya vitendo hivi yatakuwa makubwa na wananchi watashindwa kupata haki yao ya kupata huduma na msaada wa kisheria kutoka kwa mawakili iwapo vitendo hivi vitaendelea," amesema Olengurumwa

Kutokana na hilo, ameshauri kwamba ikitokea kuna wakili viongozi anadhani amekiuka maadili ya kazi yake basi atoe taarifa kwa chama cha mawakili au mahakama

Pia kwa mawakili amewasihi  kupitia vyama vyao wasimame kwa umoja na kulinda Uhuru wa kazi ya mawakili na utawala wa sheria hapa nchini

Sambamba na hilo, Mratibu huyo amewaomba wakuu wa mikoa na wilaya nchini kuacha kutumia madaraka yao chini ya kifungu cha 15 na 17 cha sheria ya Tawala za Mkkoa ya mwaka 1996 kwa kutoa amri ya kuwakamata watu na kuwaweka vizuizini bila sababu za msingi za kisheria kwani vitendo hivyo vimekuwa vokijirudia mara kwa mara.
Mtandao walaani kukamatwa kwa Wakili Arusha Mtandao walaani kukamatwa kwa Wakili Arusha Reviewed by KUSAGANEWS on August 01, 2018 Rating: 5

No comments: