Rais John Magufuli amesema hakuna mwenye uhakika wa cheo
katika serikali ya awamu ya tano hata yeye hana uhakika
Ameyasema hayo leo Agosti Mosi, wakati akihutubia mara baada
ya kuwaapisha wakuu wa mikoa, makatibu tawala, makatibu wakuu na manaibu katibu
wakuu
Amesema kazi yake ni ngumu na wakati mwingine halali usiku
au akaamshwa saa nane za usiku akipewa taarifa mbalimbali
“Hii ni kazi ngumu, kama jana usiku nimeamka saa nane usiku IGP
ananipigia simu anasema kuna watu wetu wamepata ajali mpakani, kuna mwingine
anasema hivi. Basi na nyinyi mteseke kama mimi ninavyoteseka,” amesema
Amewaambia wateule hao hakuna anayeweza kukwepa kazi
hiyo na ana uhakika wana uwezo mkubwa wa kuwatumikia wananchi
Magufuli: Urais ni kazi ngumu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 01, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 01, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment