Mwili wa
muigizaji wa vichekesho Amri Athumani 'Mzee Majuto' umewasili Donge nyumbani
kwake jana 7.05 usiku baada ya kusimamishwa katika vijiji 14 na mashabiki
wakitaka kutoa heshima ya mwisho
Safari ya
kwenda Tanga kwaajili ya mazishi ilianza saa 10.15 jioni baada ya kumuaga
katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam
Leo kuanzia
saa 5.45 mchana, ibada ya mazishi itafanyika katika msikiti wa Nuruguda uliopo
karibu na nyumbani kwake na kuzikwa kijiji cha Kiruku yalipo mashamba yake nje
kidogo cha jiji la Tanga
Mwili
ulipowasili nyumbani kwa Mzee Majuto, kuliibuka vilio huku wanawake wengi
wakizimia.
Kwa zaidi ya mwaka mmoja jina la Mzee Majuto
lilitawala vyombo vya habari likihusishwa na ugonjwa wa henia na baadaye tezi
dume
Januari mwaka
huu, Mzee majuto alifanyiwa upasuaji wa tezi dume katika hospitali ya Tumaini
jijini Dar es Salaam
Hata hivyo,
kidonda cha upasuaji wa henia kiliendelea kumsumbua na alilazwa kwa mara
nyingine katika hospitali hiyo katikati ya mwezi Aprili
Mei 4, mwaka
huu Mzee Majuto alisafirishwa kwenda India kupata matibabu katika
hospitali ya Apollo, katika Jiji la New Delhi
June 23, mwaka
huu Mzee Majuto alirejea nchini baada ya kupata matibabu yaliyokuwa
yakigharamiwa na Serikali na moja kwa moja alipelekwa katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili kwaajili ya uangalizi kabla ya kuruhusiwa na kisha kurudishwa tena
Julai 31 hospitalini hapo
Msafara wa Mzee Majuto wasimamishwa vijiji 14
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 10, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment