Mahakama ya Wilaya ya Mbozi, Songwe imemuachia huru mbunge
wa Mbozi (Chadema), Pascal Haonga na wenzake wawili baada ya kukutwa hawana
hatia katika kesi iliyokuwa ikiwakabili
Haonga na wenzake, Wilfredy Mwalusamba (katibu wake) na Mashaka
Mwampashi wameachiwa huru leo mchana Ijumaa Agosti 10, 2018
Walikuwa wakikabiliwa na mashtaka matatu ya kufanya
fujo na kuvuruga mkutano wa uchaguzi wa baraza la mji mdogo wa Mlowo,
kosa la pili na tatu ni kuwazuia askari kutekeleza majukumu yao
Akisoma huku hiyo leo hakimu mkazi Mfawidhi wa Mahakama
hiyo, Nemes Chami amesema katika mashtaka yote matatu, upande wa mashtaka
umeshindwa kuthibitisha makosa
"Katika ushihidi wa mashahidi sita wa upande wa
Jamhuri hakuna mahali walipothibitisha kwamba washtakiwa walikataa kukamatwa,”
amesema
“Hakuna mahali walipoonesha kwamba washtakiwa hawa
waliwazuia askari kutekeleza majukumu yao na hakuna mahali walipothibitisha
kwamba washtakiwa walilazimisha kurudi ukumbini baada ya kutolewa nje.”
Amesema kutokana na upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha
ushahidi wa mashtaka waliyoyawasilisha mahakamani hapo, mahakama inawaachiria
huru washtakiwa wote
Amesema kama kuna upande unaona haujaridhika na hukumu hiyo
una haki ya kukataa rufaa ndani ya muda wa kisheria
Mbunge wa Chadema aachiwa Huru
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 10, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment