Jumla ya mashahidi 34 wa upande wa mashtaka watatoa ushahidi
wao katika kesi ya mauaji ya kukusudia inayomkabili mmiliki wa Shule ya
Scolastica, Edward Shayo na wenzake wawili
Shayo pamoja mwalimu wa shule hiyo, Labani Nabiswa na mlinzi
Hamis Chacha wanatuhumiwa kumuua mwanafunzi wa kidato cha pili shuleni hapo,
Humphrey Makundi, Novemba 6, 2017
Hata hivyo katika maelezo yote yaliyosomwa jana mahakamani
hakuna shahidi aliyeshuhudia mauaji hayo isipokuwa maelezo ya kukiri kosa ya
mshtakiwa wa pili pekee, Chacha
Maelezo hayo yalisomwa kuanzia nne asubuhi hadi saa tisa
alasiri na wakili wa Serikali mwandamizi wa Serikali, Omary Kibwana
aliyesaidiana na Lilian Kiweo na Nitike Emmanuel
Katika maelezo yake ya ungamo anayodaiwa kuyatoa mbele ya
mlinzi wa amani ambaye ni Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo, Irene Mushi, mshtakiwa
huyo anadaiwa kukiri kumuua mtoto huyo
Mlinzi huyo anaeleza katika maelezo hayo kuwa, Humphrey
aliruka ukuta na wakati anamkimbiza alimpiga na ubapa wa panga mgongo na mara
ya pili alimpiga usoni akaanguka
Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Moshi, Julieth Mawolle,
wakili huyo anaeleza kuwa baada ya kuanguka na kuhisi amefariki, mshtakiwa
alimjulisha Nabiswa na baadaye alikuja Shayo na kusema kuwa mwili wa mwanafunzi
huyo ukatupwe mtoni
Maelezo ya mpelelezi mkuu wa kesi hiyo, Inspekta Waziri
Tenga yanaeleza kuwa hakuna ubishi kuwa Shayo na Nabiswa walihusika kuficha taarifa
hata baada ya kuokotwa kwa mwili
Inspekta Tenga anaeleza katika maelezo hayo kuwa wakati
mshtakiwa alipohojiwa na polisi, alikiri kumuua mwanafunzi huyo kwa kumpiga kwa
ubapa la panga mgongoni na usoni
Maelezo mengine yote ya mashahidi yanaeleza namna mwili huo
ulivyogunduliwa mtoni, kuopolewa, kupelekwa hospitali ya mkoa ya Mawezi na
baadaye kuzikwa na halmashauri
Mbali na hilo, maelezo ya mashahidi wengine yanaeleza namna
mwili wa mtoto huyo ulivyofukuliwa na kufanyiwa uchunguzi (postmoterm) katika
Hospitali ya KCMC
Pia upo ushahidi wa mtaalamu kutoka ofisi ya Mkemia Mkuu wa
Serikali, Hadija Mwema ambaye alichunguza sampuli zilichokuliwa kwenye mwili
uliofukuliwa na kuzioanisha na za wazazi wake
Kwa upande wake, baba mzazi, Jackson Makundi katika maelezo
yake anaeleza namna alivyopata taarifa za mwanaye kutokuwwpo shuleni kuanzia
Novemba 7, 2017 na jitihada za kumtafuta. Kesi hiyo iliahirishwa
Mashahidi 34 kutoa ushahidi dhidi mauaji mwanafunzi Scolastica
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 04, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 04, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment