Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla
ameondolewa katika hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center na kuhamishiwa
jijini Dar es Salaam kwa matibabu zaidi
Dk Kigwangalla amepata ajali leo Jumamosi Agosti 4, 2018
eneo la Magugu mkoani Manyara na kupata majeraha sehemu mbalimbali mwilini
Katika ajali hiyo ofisa habari wa wizara hiyo, Hamza Temba
amefariki dunia
Akizungumza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Meja Jenerali
Gaudence Milanzi amesema licha ya waziri huyo kuendelea vizuri, anahitaji
matibabu zaidi
Amesema ndege itakayomchukua waziri huyo ipo Arusha na
kwamba ataambatana na watu kadhaa
Kuhusu mazishi ya Temba, amesema yatafanyika kesho saa
saba mchana nyumbani kwao Masama wilayani Hai mkoani Kilimanjaro
Dk Kigwangalla aliondolewa katika hospitali hiyo akiwa
pamoja na Milanzi, mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na Waziri wa Madini,
Angellah Kairuki
Awali, waziri huyo alipatiwa matibabu katika kituo cha
afya cha Magugu na kuhamishiwa hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center kwa
helkopta
Dk Kigwangalla ahamishiwa Dar
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 04, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment