Ajali yaua watatu Pwani


Watu watatu wamefariki dunia mkoani Pwani, wawili kati yao katika ajali ya basi iliyojeruhi wengine wanane

Basi hilo mali ya kampuni ya Modern Coach lililokuwa likitokea Nairobi kwenda Dar es Salaam, liliacha njia na kupinduka

Ajali hiyo imetokea jana Ijumaa Agosti 3, 2018 saa 5.45 usiku katika Kijiji cha Kimange kwenye barabara ya Segera – Chalinze

Akizungumza leo Jumamosi Agosti 4, 2018, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Blasius Chatanda amewataja waliofariki dunia kuwa ni Aliakimu  Mkiganda (41) mfanyabiashara ambaye ni raia wa Rwanda na Emmanuel Indimuli (3) raia wa Kenya. Miili yao imehifadhiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH

Amesema majeruhi katika ajali hiyo ni Penina Wango (33), Aliasgher Morbiwalia (18), Adrian Flovick (19), Mohamed Idris (18)  Mita Naidhukum (54), Adrin Maula (16), Erick Muthon (30) na Hemik  Muthon (49) wote raia wa Kenya

Amesema majeruhi wote walipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu

Amesema dereva wa basi hilo amekimbia na juhudi za kumsaka zinaendelea ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake

Katika tukio jingine, amesema mwendesha pikipiki Idd Bakar (20), amefariki dunia baada ya kugongana na basi mali ya kampuni ya ABC lililokuwa linatokea Dar esalaam kwenda Mailimoja, Kibaha
Ajali yaua watatu Pwani Ajali yaua watatu Pwani Reviewed by KUSAGANEWS on August 04, 2018 Rating: 5

No comments: