Ubalozi wa Marekani umetoa tamko kuhusu uchaguzi mdogo wa
jimbo moja na kata 77 uliofanyika Jumapili, ukieleza umepata taarifa za
kuaminika kwamba ulighubikwa na vurugu na ukiukwaji wa sheria.
Taarifa iliyotolewa leo Agosti 15 kwa vyombo vya habari na
Ofisi ya Habari ya Ubalozi huo, imeeleza kuwa ukiukwaji wa sheria katika
uchaguzi huo ulihusisha kukataa kwa baadhi ya watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
kuwasajili wagombea kutoka vyama vya upinzani
Pia taarifa hiyo imeeleza vitisho vya polisi dhidi ya
wanachama wa vyama vya upinzani, watu kukamatwa kiholela bila kuwapo vibali vya
ukamataji vilitawala katika uchaguzi huo wa marudio uliofanyika Agosti 12, 2018
Pamoja na hiyo pia imeelezwa kuwa kulikuwepo na
ukandamizwaji wa uhuru wa kukusanyika na kutoa maoni katika kipindi chote cha
kuelekea uchaguzi huo. "Mambo haya yanakwaza haki ambazo Katiba ya
Tanzania imewapa raia wake na kuhatarisha amani, utulivu na usalama nchini na
eneo lote la kanda," imeeleza taarifa ya ubalozi huo
MAREKANI"Yatoa Kauli Kuhusu Uchaguzi Mdogo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 15, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment