Kesi ya aliyempa Waziri Lukuvi rushwa yagonga mwamba


Upelelezi wa kesi inayomkabili mfanyabiashara anayetuhumiwa kutaka kumpa rushwa ya Sh90 milioni Waziri William Lukuvi, bado haujakamilika

Mfanyabiashara huyo, ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Kiluwa Steal Group and Co. Ltd na Kiluwa Free Processing Zone anadaiwa kutaka kumpa rushwa hiyo Lukuvi ambaye ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hayo yameelezwa leo Agosti 15 na Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Maghela Ndimbo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huduma Shahidi wakati kesi hiyo ilipotajwa

Wakili Ndimbo amedai mahakamani hapo kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba kesi ilipangwa kwa ajili ya kutajwa na akaomba ipangiwe tarehe nyingine ili kuangalia kama ushahidi utakuwa umekamilika au la

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Shahidi aliiahirisha kesi hiyo hadi Septemba 14, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa

Mshtakiwa huyo ambaye yupo nje kwa dhamana

Katika kesi hiyo mshtakiwa huyo anadaiwa kuwa Julai 16, mwaka huu kati ya saa 6 na saa 8 mchana akiwa mkurugenzi wa kampuni hizo mbili alitoa rushwa ya Dola 40,000 za Marekani ( Sh90 milioni) kwa Waziri Lukuvi

Kesi ya aliyempa Waziri Lukuvi rushwa yagonga mwamba Kesi ya aliyempa Waziri Lukuvi rushwa yagonga mwamba Reviewed by KUSAGANEWS on August 15, 2018 Rating: 5

No comments: