Mapato madogo Dar yamuumiza kichwa Makonda


Unaweza kusema mkoa wa Dodoma kuongoza kwa mapato kati ya majiji sita yaliyopo nchini kumemtikisa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Paul Makonda

Leo Ijumaa Agosti 3, 2018 Makonda amemtaka katibu tawala wa mkoa huo, Abubakar Kunenge kukutana na wakurugenzi wa halmashauri zote za jiji hilo kupitia taarifa za mapato ili kubaini sababu za Dar es Salaam kupitwa na Dodoma katika ukusanyaji wa mapato

Ametoa kauli hiyo katika hafla ya kuwakaribisha wakuu wa wilaya wapya na kuwaaga waliohamishwa vituo vya kazi

Makonda amesema lazima wakurugenzi wa Dar es Salaam waongeze vyanzo vya mapato, kusimamia taarifa za mapato katika halmashauri zao

"Haiingii akilini tumezidiwa na Dodoma kwenye ukusanyaji wa mapato, tutafanya kila namna kurejea katika nafasi yetu," amesema Makonda akimueleza Kunenge aliyechukua nafasi ya Theresia Mbando aliyehamishiwa mkoa wa Pwani
Mapato madogo Dar yamuumiza kichwa Makonda Mapato madogo Dar yamuumiza kichwa Makonda Reviewed by KUSAGANEWS on August 03, 2018 Rating: 5

No comments: