Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Waziri wa Ardhi, Nyumba
na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi atakwenda katika Halmashauri ya Manispaa
ya Tabora kutatua kero kubwa za ardhi.
Pia, Majaliwa amezitaka wilaya zote kuhakikisha zinakuwa na
shule moja ya kidato cha tano na sita kila tarafa nchini na Serikali itapeleka
walimu.
Ameyasema hayo jana jioni Agosti 18, 2018 wakati akizungumza
na wananchi wa manispaa hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye
uwanja wa Chipukizi.
Majaliwa aliyasema hayo baada ya wabunge na wananchi kueleza
changamoto kubwa zinazowakabili ikiwamo ya migogoro ya ardhi iliyodumu muda
mrefu.
“Waziri wa Ardhi atakuja hapa na ramani zake, atakutana na
watendaji na kumaliza matatizo yote makubwa ya ardhi na yale madogo madogo
yatashughulikiwa na mkuu wa wilaya,” amesema Majaliwa.
Kuhusu ujenzi wa shule, Majaliwa amesema uwapo wa shule hizo
utaamsha ari ya wanafunzi kusoma kwa bidii, jambo litakaloongeza idadi ya
wanaoendelea na masomo ya kidato cha tano na sita.
Pia, Waziri Mkuu aliwaagiza watendaji wote kuanzia
halmashauri hadi vijiji wawasimamie wanafunzi wa kike na wahakikishe wanamaliza
masomo bila ya kukatishwa.
“Huu ni mkakati wa taifa tunataka watoto wa kike wote
walindwe ili waweze kumaliza shule na marufuku kukatisha elimu yao, iwe kwa
kuwapa ujauzito au kuwaoa, adhabu yake ni kali,” amesema.
Majaliwa jana jioni alimaliza ziara yake ya kikazi ya siku
tatu mkoani Tabora baada ya kufanya ziara wilaya za Igunga, Nzega na Manispaa
ya Tabora
Lukuvi akabidhiwa kero za ardhi Tabora
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 19, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment