Waziri wa
Mambo ya Ndani, Kangi Lugola ametoa wiki moja kwa polisi wilayani Bunda
mkoani Mara kuwakamata wanafunzi watoro na wazazi wao.
Pia, agizo hilo litawakumba watu waliowarubuni
wanafunzi wa kike na kuwasababishia kukatisha masomo
Lugola ambaye
pia ni Mbunge wa Mwibara ametoa kauli hiyo jana jioni Alhamisi Agosti 16, 2018
mkoani humo na kubainisha kuwa anasikitishwa na idadi kubwa ya wanafunzi
walioacha shule wilayani humo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kurubuniwa
na wanaume
Amesema
kiwango cha wanafunzi kuacha masomo kinazidi kuongezeka hivyo Serikali
haiwezi kukaa kimya, lazima ifanye kitu kuhakikisha wanafunzi hao wanasoma ili
waje kuwa viongozi wa nchi
“Mkuu wa Polisi
hapa Bunda, nawapa wiki moja, mtumie elimu zenu za upelelezi mliofundishwa,
wakamateni, wachunguzeni, wahojini ndugu, jamaa, majirani mtawapata wote
wanaowarubuni watoto hawa, halafu mushughulike nao,” amesema Lugola.
Lugola: Polisi wakamateni wanafunzi watoro
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 17, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment