Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola ametoa siku 15 kwa
kampuni saba zilizobainika kufanya ufisadi katika mradi wa mfumo wa utambuzi wa
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), kurejesha Sh28.5bilioni walizolipwa
Amezitaka kampuni hizo kutekeleza agizo hilo ili kuepuka
kuwa wateja wa mahakama ya mafisadi
Ufisadi huo uligundulika katika ukaguzi uliofanywa na
Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA), Februari, 2016
Ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Agosti 4, mjini Dodoma ikiwa
ni siku moja baada ya kukutana na wamiliki wa kampuni hizo kuomba wawasilisha
vielelezo vya malipo hayo
Lugola amezitaja kampuni hizo na kiasi cha fedha katika
mabano kuwa ni Gotham International Ltd (Sh2.8 bilioni), Iris Corporation
Berhard (Sh22.9 bilioni), Gwiholoto impex Ltd (Sh 946.4 milioni
Nyingine ni Skyes Travel Agent (Sh6 milioni), Dk Shija Paulo
Rimoy (Sh27 milioni), Aste Insurance (Sh1.2 bilioni) na BMTL (Sh 569.1 milioni)
ambayo imekubali kurejesha fedha hizo
Lugola amesema wamiliki hao na watu wengine wanaopata zabuni
kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Serikali wanatakiwa kutofanya ufisadi
kupitia kivuli cha mikataba
“Ninawaomba msicheze na Serikali ya Awamu ya Tano kwa sababu
imeapa kulinda rasilimali za Watanzania. Kuna mahakama ya mafisadi,” amesema
“Takwimu nilizonazo mahakama ile bado ina uhaba wa
mafisadi, mimi nina dhamana ya kuitafutia wateja. Nyinyi tuliohojiana leo
muombe msiwe miongoni mwa wateja ninaoitafutia mahakama hiyo.”
Kuhusu hatima ya aliyekuwa mkurugenzi wa Nida, Dickson Maimu
na kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malasia ambayo ililipwa Sh32
bilioni na Nida kwa ajili ya kuleta mtambo wa kutengenezea kadi ghafi nchini,
amesema itajulikana Agosti 17, 2018
“Maimu yeye ametusaidia kupata maelezo ya ziada kuhusu ile
kampuni, baada ya siku 14 watakavyokuja ndio tutajua hatima yake, tutajua kama
suala litaisha ama la,” amesema Lugola
Amesema Maimu na mmiliki wa kampuni ya Jack Ghotham
waliitika wito wake jana na kutoa maelezo ya ziada ambayo yatawasaidia katika
kutafuta ufumbuzi wa suala hilo
Julai 25, 2018 Lugola aliipa wiki mbili kampuni ya Iris na
Ghotham kwenda ofisini kwake kujadiliana jinsi ya kumaliza suala hilo
Lugola azibana kampuni, ataka zirejeshe Sh28.5 bilioni
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 04, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 04, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment