Dar es Salaam. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi
Kigwangalla amewasili katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu
zaidi
Ndege iliyombeba waziri huyo imetua katika Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 12 jioni, msafara kuondoka kuelekea
Muhimbili
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dk Mpoki Ulisubisya na
mkurugenzi mtendaji wa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru pamoja na jopo
la madaktari wamempokea Dk Kigwangalla katika kitengo cha magonjwa ya
dharura Muhimbili
Dk Kigwangalla amepata ajali leo Jumamosi Agosti 4, 2018
eneo la Magugu mkoani Manyara na kupata majeraha sehemu mbalimbali mwilini
Awali, waziri huyo alipatiwa matibabu katika kituo cha
afya cha Magugu na kuhamishiwa hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center kwa
helkopta
Katika ajali hiyo ofisa habari wa wizara hiyo, Hamza Temba
amefariki dunia
Dk Kigwangalla awasili Muhimbili
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 04, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 04, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment