Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili mshtakiwa Habinder
Seth na mwenzake, leo Alhamisi 16, 2018 imeahirishwa katika mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu hadi Agosti 30, 2018
Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Kelvin Mhina ameahirisha
kesi hiyo leo hadi Agosti 30, 2018 baada ya wakili wa Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai kueleza upelelezi wa kesi hiyo
bado haujakamilika
Swai ameomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya
kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la
Hata hivyo, Hakimu Mhina amesema kesi hiyo imeahirishwa kwa
kuwa hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi anayeiendesha kesi hiyo anaumwa
Mbali na Seth, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni
mfanyabiashara, James Rugemalira, ambao kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12,
katika Mahakama hiyo
Mashtaka hayo ni uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha
mtandao wa uhalifu, kuhushi, kutoa nyaraka za kughushi
Pia wanadaiwa kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu na
kutakatisha fedha
Kesi ya Seth, Rugemalira yakwama tena
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 16, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment