Unaweza kusema halmashauri ya Monduli Mkoa wa Arusha
ambayo ilikuwa inaongozwa na Chadema imerejea CCM baada ya madiwani 10 wa chama
hicho kikuu cha upinzani nchini kujiuzulu na kujiunga na chama tawala
Akizungumza leo Jumamosi Agosti 11, 2018 mkurugenzi wa
halmashauri hiyo, Steven Ulaya amesema baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015,
Chadema walipata madiwani 18, wakiwemo wa viti maalum watano huku CCM ikipata
madiwani tisa, wawili wakiwa wa viti maalum
“Tayari CCM imeshinda kata sita katika chaguzi ndogo za
udiwani zilizofanyika, bado kuna uchaguzi katika kata mbili, ikiwemo ya Monduli
baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo kujiuzulu. Pia aliyekuwa
mbunge (wa Chadema Monduli-Julius Kalanga) amejiuzulu,” amesema
Amesema kwa sasa Chadema imebaki na madiwani tisa,
wakiwemo watano wa viti maalum
Akizungumza wimbi la madiwani kujiuzulu, Katibu wa
Chadema Mkoa wa Arusha, Aman Golungwa amesema kinachofanywa na wanaohama ni
mchezo mchafu, kusisitiza kuwa chama hicho hakiwezi kufa, “waache waondoke ila
wananchi wanajua kinachoendelea.”
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema
wanaotaka kuondoka katika chama hicho wasijifiche, kuwataka watoe taarifa na
wataagwa
“Tunasema waache waondoke kwa ajili ya shida zao binafsi
sisi tutabaki na kamwe wasidhani Chadema itakufa,” amesema
Mpaka sasa madiwani 31 wa Chadema mkoa wa Arusha
wamejiuzulu na kujiunga na CCM.
Halmashauri Monduli Rasmi Kurejea CCM kutokana na Hili.
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 11, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment