Chadema wamfuta uanachama diwani wake Mbeya


Kamati tendaji ya Chadema Wilaya ya Mbarali(Mbeya)  imemfuta uanachama na kumvua udiwani, Diwani wa Kata ya Ruiwa, Kassim Mtale kwa madai utovu wa nidhamu, usaliti na kukiuka taratibu na kanuni za chama hicho

Akizungumza Katibu wa Chadema Wilaya ya Mbarali, Nicolaus Lyaumi amesema katika kikao chao walichoketi Alhamisi wiki hii walijiridhisha kwamba Mtale amekiuka taratibu za chama hicho, hivyo wakakubaliana kumfuata uanachama na kumvua udiwani

"Kweli tulishamfuta uanachama na kumvua udiwani, kuna mambo mengi yalifanyika dhidi yake ya usaliti, utovu wa nidhamu, sasa Chadema ni taasisi ya umma sio mtu mmoja. Kutokana na hayo chama kimeamua kumfuta kabisa uanachama," amesema Lyaumi

Hata hivyo, Mtale mwenyewe kasema hajafukuzwa ila amejivua uanachama na udiwani kwa hiyari yake na kujiunga na CCM.

Amesema ameamua kwenda CCM akiamini kwamba huko ataweza kuwatumikia vyema wanannchi wake tofauti na akiwa Chadema au chama chochote cha upinzani

Amesema; ‘Sisi vijana tuliingia huku (Chadema) tukiwa na matumaini makubwa kwamba kutakuwa na fursa nyingi, lakini nimeona yale yote tuliyokuwa tunayahubiri ndiyo yanayotekelezwa na Rais wetu John Magufuli. Hivyo na mimi sina budi kumfuata ili kuongeza nguvu zaidi”

Chadema wamfuta uanachama diwani wake Mbeya Chadema wamfuta uanachama diwani wake Mbeya Reviewed by KUSAGANEWS on August 11, 2018 Rating: 5

No comments: