Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa na
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Halima Mdee (Mb) pamoja na viongozi wengine,
wanachama na wapenzi wa CHADEMA Jimbo la Kawe takribani 13, wamekamatwa na
wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Polisi Kawe.
Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara
ya Habari na Mawasiliano CHADEMA, Tumaini Makene imesema kwamba hadi
sasa jeshi hilo halijatoa taarifa rasmi kueleza sababu ya kumshikilia mbunge
huyo pamoja na wananchi wake baada ya kuwakamata maeneo ya Tanganyika Parkers,
Kawe, jijini Dar es Salaam.
Akielezea kuhusu Mdee kukamatwa
Makene amesema kwamba, "awali, Mdee ambaye ni mbunge wa Jimbo la Kawe,
alisimamishwa na wananchi alipopita maeneo hayo, wakitaka kumpatia kero zao.
Baada ya kusikiliza malalamiko ya wapiga kura wake na kuondoka, inadaiwa polisi
walifika eneo hilo na kuanza kuwakamata walioonekana kuwa na sare za
CHADEMA".
Ameongeza kwamba alipopata taarifa
hizo, Mdee alilazimika kurudi ambapo polisi hao wakiongozwa na askari polisi
mwenye cheo cha Inspekta walimuamuru Mdee na viongozi hao kuelekea kituoni.
Hadi sasa viongozi hao bado wako kituoni hapo".
Hata hivyo juhudi zinafanyika za
kuweza kuzungumza na jeshi la Polisi Kawe ili kujua sababu za viongozi na
wananchi hao kukamatwa
Halima Mdee awaponza wananchi wake
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 01, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 01, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment