Dc Longido "Wananchi wa Longido Chukueni Tahadhari Kuhifadhi Chakula"


Serikali imewataka Wananchi wa Wilaya ya Longido Mkoani Arusha kuchukua Tahadhari mapema kwa kuwa na tabia ya Kuhifadhi chakula ili kipindi cha Ukame wasilie njaa kwa kuwa Wilaya hiyo imebarikiwa kuwa na maeneo ambayo ni mazuri kwa kilimo na ufugaji.

Hayo yamesema na mkuu wa wilaya ya Lingido Mh Frank Mwaisumbe wakati alipotembelea na kukagua Ghala la Kuhifadhia nafaka katika tarafa ya Engarenaibo mradi ambao umegharimu  zaidi ya Shilingi Milioni 100 mpaka ulipokamilika ambapo unasubiria Mwenge kwa ajili ya kuzinduliwa.
.
Mwaisumbe amesema kuwa serikali inahakikisha inajali wananchi wake ndiyo mana ikatoa Fedha hizo ili kuleta mradi huo ambapo amewaomba wananchi kutumia Fursa Hiyo ambayo inaletwa na Serikali ya awamu ya Tano Chini ya Raisi Dkt John Pombe Magufuli.

Amesema kuwa mradi huo  utawasaidia wananchi kioindi cha ukame pamoja na kupunguza gharama kubwa ya kununua Chakula .

Ameongea kuwa licha ya kuwa jamii inayoishi wilayani Longido Wengi ni Wafugaji ni vema wakatumia Fursa ya Kununua Chakula na Kuhifadhi kwa kuuza baadhi ya Mifugo ambayo italeta faida kwa kuwa na chakula kuliko kusubiri kipindi cha Ukame ambacho Mifugo ufariki kwa Kukosa Malisho.


Dc Longido "Wananchi wa Longido Chukueni Tahadhari Kuhifadhi Chakula" Dc Longido "Wananchi wa Longido Chukueni Tahadhari Kuhifadhi Chakula" Reviewed by KUSAGANEWS on August 18, 2018 Rating: 5

No comments: