Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya
ameamuru kukamatwa kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Tudeley Estates Ltd, Jensen
Natal na Mwanasheria wa kampuni hiyo, Edward Mroso kwa tuhuma za kukwepa kodi
ya serikali kiasi cha zaidi ya Sh800 milioni
Pia ameiamuru Idara ya Uhamiaji Wilayani humo kumnyang'anya
hati ya kusafiria meneja wa kampuni hiyo, Trevor Gifford hadi fedha hizo
zitakapolipwa.
Kampuni ya Tudeley
inamiliki na kuendesha mashamba ya ushirika ya chama cha msingi cha Murososangi
yenye ukubwa wa ekari 2,054.
Ole Sabaya, ametoa
maagizo hayo leo Agosti 16 wakati alipofanya ziara ya kutembelea mashamba ya
kampuni hiyo huku akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama Wilayani Hai
Pia aliambatana na Meneja wa Mamlaka ya Mapato (TRA)
wilayani Hai, Spécioza Owere
Kabla ya kuingia katika lango kuu la kampuni hiyo Ole Sabaya
aliamuru Gifford aitwe huku akiwa na hati yake ya kusafiria na baadaye
akaingia katika ofisi za kampuni hiyo
Akizungumza katika eneo la tukio, Ole Sabaya amesema kwamba
ana taarifa za uhakika kwamba kampuni hiyo imekuwa ikikwepa kulipa kodi
ya serikali kwa muda wa miaka saba hadi sasa
Ole Sabaya amesema kwamba kampuni hiyo imekwepa kulipa kodi ya
serikali zaidi ya Sh800 milioni ambazo ni malimbikizo ya kodi ya Mamlaka ya
Mapato nchini (TRA
Akitoa maagizo hayo Ole Sabaya aliliamuru jeshi la polisi
Wilayani humo kumkamata Natal na Mroso na kuwekwa mahabusu kwa saa
48 na wahakikishe fedha hizo ambazo ni kodi ya serikali zinalipwa
"Wewe utaenda ndani ili uje uniambie kuna utaratibu
gani wa kodi ya serikali kulipwa na ijumaa asubuhi uwepo ofisini kwangu
uniambie kodi ya serikali italipwaje,” amesema kuongeza
"Chukua passport yake ya zamani na sasa nataka pésa
hiyo ilipwe ndani ya siku saba na TRA niletewe maelezo hayo.”
Mara baada ya agizo hilo maofisa wa jeshi jeshi la Polisi
Wilayani humo walimkamata Natal na Mroso na kisha kuwapéleka kwenye gari huku
maofisa wa idara ya Uhamiaji wakichukua hati ya kusafiria ya Trevor
Kabla ya Mroso kushikiliwa alimweleza Ole Sabaya kwamba
uongozi wa kampuni hiyo ulishawasilisha maombi mbele ya ofisi yake kuwaomba TRA
wakague hesabu na madeni ili waweze kulipa
Dc Hai agawa Kifurushi cha Masaa 48 Kwa Boss na Mwanasheria wa Kampuni ya Tudeley Estates Ltd
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 16, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment