Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) leo mchana Jumapili Agosti 12, 2018
wametangaza kujitoa katika uchaguzi kata ya Songoro wilayani Arumeru kwa madai
kuwa mawakala na mgombea wao wamepigwa na vijana wanaodaiwa kuwa makada wa CCM
Akizungumza leo
mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari amesema baada ya mashauriano
kati ya chama na mgombea, Godluck Nanyaro wameona hakuna sababu ya kuendelea na
uchaguzi
“Tumeamua
kuwaondoa vituoni mawakala wetu katika vituo 14 kutokana na kuwepo kwa
ukiukwaji mkubwa wa taratibu,” amesema
“Mgombea
amepigwa, mawakala wanapigwa vituoni na wengine walizuiwa kuingia vituoni
muda mrefu huku upigaji kura ukiendelea
Nassari akiwa
pamoja na Katibu wa Chadema mkoa Arusha, Isaya Mungure amesema mapema leo
asubuhi katika eneo la Shule ya Msingi Urisho, mawakala wao walizuiwa
Amebainisha
kuwa Nanyaro alikwenda kushuhudia hali hiyo katika kituo cha Urisho A
lakini alivamiwa na vijana aliodai ni wa CCM na kumshushia kipigo jambo
lililowalazimu polisi kuingilia kati na kuwapeleka wote kituoni
Msimamizi
uchaguzi Arumeru Mashariki, Christopher Kazeri amesema Chadema waliondoa
mawakala wao saa 5 asubuhi bila kueleza sababu za kujitoa
Amesema vyama
vina hiari ya kujitoa lakini hatua hiyo haipotezi uhalali wa uchaguzi kuendelea
Kuhusu mgombea
wa Chadema kupigwa, msimamizi huyo wa uchaguzi amesema alishushiwa kipigo kwa
kuwa alikwenda kupigana na mawakala wa CCM na polisi kumkamata
Chama cha Chadema wajitoa uchaguzi Songoro jijini Arusha
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 12, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment