Jeshi la polisi mkoani Arusha limefungua jalada la uchunguzi
wa matukio ya vurugu katika uchaguzi kata ya Kaloleni jijini Arusha baada ya
watu wawili kuchomwa visu huku mbunge wa Arusha mjini (Chadema), Godbless Lema
akishushiwa kipigo
Akizungumza leo
Jumapili Agosti 12, 2018 kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi
amesema Lema ametoa taarifa za kushambuliwa sambamba na mgombea wa chama hicho
katika kata hiyo, Boniface Kimario pamoja na wakala wake
Amesema baada ya taarifa hiyo, majeruhi walipelekwa katika
hospitali ya mkoa ya Mount Meru wanakoendelea na matibabu
“Tumefungua jalada la uchunguzi na tunawasaka waliohusika,”
amesema
Katika tukio hilo, Lema anadaiwa kushushiwa kipigo na watu
wanaodaiwa kuwa walinzi wa CCM wakimtuhumu kutaka kufanya vurugu eneo la Tangi
la Maji
Mbali na Lema, wakala wa Chadema, Ibrahim Ismail amechomwa
visu na kulazwa katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru
Katika vurugu hizo, pia inadaiwa mwenyekiti wa CCM kata ya
Kaloleni, Iddi Mukuru amejeruhiwa kwa kuchomwa visu
Akizungumza mgombea wa CCM katika kata hiyo, Emmanuel Kessy
amesema licha ya vurugu hizo uchaguzi unakwenda vizuri, “ingawa watu wachache
wamejitokeza ila uchaguzi unakwenda vizuri.”
Katika Jiji la Arusha unafanyika uchaguzi katika kata nne
baada ya waliokuwa madiwani wa Chadema kujiuzulu na kuhamia CCM ambako
wamepitishwa kuwania tena nafasi hiyo kwa tiketi ya chama hicho tawala
Jeshi la polisi mkoani Arusha limefungua jalada la uchunguzi
wa matukio ya vurugu katika uchaguzi kata ya Kaloleni jijini Arusha baada ya
watu wawili kuchomwa visu huku mbunge wa Arusha mjini (Chadema), Godbless Lema
akishushiwa kipigo
Akizungumza leo
Jumapili Agosti 12, 2018 kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi
amesema Lema ametoa taarifa za kushambuliwa sambamba na mgombea wa chama hicho
katika kata hiyo, Boniface Kimario pamoja na wakala wake
Amesema baada ya taarifa hiyo, majeruhi walipelekwa katika
hospitali ya mkoa ya Mount Meru wanakoendelea na matibabu
“Tumefungua jalada la uchunguzi na tunawasaka waliohusika,”
amesema
Katika tukio hilo, Lema anadaiwa kushushiwa kipigo na watu
wanaodaiwa kuwa walinzi wa CCM wakimtuhumu kutaka kufanya vurugu eneo la Tangi
la Maji
Mbali na Lema, wakala wa Chadema, Ibrahim Ismail amechomwa
visu na kulazwa katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru
Katika vurugu hizo, pia inadaiwa mwenyekiti wa CCM kata ya
Kaloleni, Iddi Mukuru amejeruhiwa kwa kuchomwa visu
Akizungumza mgombea wa CCM katika kata hiyo, Emmanuel Kessy
amesema licha ya vurugu hizo uchaguzi unakwenda vizuri, “ingawa watu wachache
wamejitokeza ila uchaguzi unakwenda vizuri.”
Katika Jiji la Arusha unafanyika uchaguzi katika kata nne
baada ya waliokuwa madiwani wa Chadema kujiuzulu na kuhamia CCM ambako
wamepitishwa kuwania tena nafasi hiyo kwa tiketi ya chama hicho tawala
Vurugu zaibuka Kwenye Marudio ya uchaguzi Mdogo Jijini Arusha, Polisi wachunguza
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 12, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment