Idara ya Uhamiaji inadaiwa kuishikilia pasipoti ya
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze
Pamoja na hatua hiyo, Eyakuze amewaambia waandishi wa habari
leo Agosti 3 kwamba suala hilo halitawayumbisha, bali taasisi hiyo itaendelea
na kazi zake kama kawaida
"Niliombwa nifike Uhamiaji na kupeleka pasi,
nikatekeleza, lakini mpaka leo sijapata maelezo wala barua ya kwa nini
washikilie pasi yangu," amesema Eyakuze
Amesema baada ya pasi ya kusafiria kushikiliwa, aliomba pasi
ya muda kwa ajili ya safari ya kwenda Nairobi kikazi lakini pia alinyimwa,
"Hatujapata taarifa ya kuwepo kwa kesi mahakamani," ameongeza
Amesema walipokea barua mbili zikihoji kwa nini
wasichukuliwe hatua na wakazijibu
Ingawa hakutaka kuingia undani wa baru hizo, Julai 5, Tume
ya Sayansi na Teknolojia (Costech), iliiandikia barua Twaweza ikiitaka itoe
maelezo ndani ya siku saba kuhusu utafiti iliofanya wa Sauti za Wananchi bila
ya kibali.
Utafiti huo pamoja na mambo mengine umeonesha kushuka kwa
uungaji mkono wa wananchi kwa wawakilishi na viongozi waliowachagua
"Hatutishiki kwa kuitwa na kuhojiwa na Serikali lakini
tunadhani ni haki yao kuhoji na sisi kama wajibu wetu kuwajibu. Kwa sababu
sheria inaeleza wazi ni tafiti tunazofanya,” amesema
Msemaji wa Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanda amesema hana
taarifa ya kushikiliwa kwa pasi ya kusafiria ya Eyakuze
"Bado sijapata hizo taarifa, niko nje ya Dar es salaam,
nikirudi nitaifanyia kazi," amesema
Utafiti huo pia ulionyesha kuporomoka kwa ukaribu wa
wananchi na vyama vya siasa, utekelezaji wa majukumu kwa viongozi walioko
madarakani, Rais anavyotekeleza majukumu yake tangu alipoingia madarakani na
uhuru wa kujieleza katika baadhi ya maeneo
Julai 11, Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech)
iliiandikia barua Twaweza na kuitaka kutoa maelezo kuhusu kibali cha kufanya
utafiti huo
Bosi Twaweza adai Uhamiaji wamemnyang’anya pasipoti
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 03, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 03, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment