Dar es Salaam. Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za
Kulevya (DCEA) inamshikilia mkazi wa Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam,
Mohamed Hussein Gulam (48) kwa tuhuma za kukutwa na gramu 300 za dawa za
kulevya zinazodhaniwa kuwa ni heroin
Kamishna wa Intelijensia wa mamlaka hiyo, Fredick Kibuta
amezungumza akisema mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti 16, 2018 saa 9 usiku
nyumbani kwake akiwa na dawa hizo alizokuwa akiziandaa kwa ajili ya kuziuza
Amesema baada ya kuzikamata walifanya vipimo vya awali na
kuonyesha unga huo ni dawa za kulevya aina ya heroin hivyo wameupeleka kwa
mkemia mkuu wa serikali ili kubaini aina gani ya dawa za kulevya iliyokamatwa
"Mtuhumiwa bado tunamshikilia tunasubiri majibu kutoka
kwa mkemia mkuu wa Serikali yakikamilika hatua za kisheria zitachukuliwa
ikiwemo kufikishwa mahakamani," amesema Kibuta
Amesema Gulam alianza biashara ya kuuza dawa za kulevya aina
ya heroin mwaka 1995 akiwa anaishi nchini Italia ambapo alikuwa akiagiza dawa
hizo nchini Pakistani na kuzisambaza nchi mbalimbali
Mwaka 1999 alirudi nchini huku akiendelea na biashara hiyo
na alikuwa akishirikiana na washirika wake kutoka Nigeria alikokuwa anauza kwa
rejareja na jumla
Amezitaja baadhi ya
nchi alikokuwa anaziuza dawa hizo kuwa ni Uturuki, Italia, Afrika Kusini,
India na Kenya huku akiwatumia watu wake ambao walikuwa wanasambaza
Kibuta amesema Julai 18, 2018, mamlaka hiyo ilimkamata mkazi
wa Kagera jijini Dar es Salaam, Islem Shebe Islam akiwa na gramu 306 za heroin,
Julai 20, 2018 alikamatwa mkazi wa Ununio jijini humo, Mfungeni Azizi Mohamed
akiwa na gramu 215 aina ya heroine na gramu 3.15 aina ya cocaine na Agosti 14,
2018 alikamatwa Ally Yusuph maarufu Porojo akiwa na gramu 300 za dawa aina ya
heroin
Anaswa na Gramu 300 za dawa za Kulevya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment