Zitto, Polepole wavutana mtandaoni kisa Mwigulu


Mambo yamekuwa mambo mitandaoni. Ndivyo unavyoweza kusema kutokana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe kuvutana katika mtandao wa kijamii wa Twitter kuhusu mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri

Katika mabadiliko hayo yaliyofanywa na Rais John Magufuli, Mwigulu Nchemba ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ameachwa

Zitto aliandika katika ukurasa wake, “ndugu yangu Mwigulu Nchemba karibu back bencha ufanye kazi ya wananchi. Tunajua msimamo wako kuhusu barua ya KKKT (Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania) umekuponza, ulikuwa na msimamo madhubuti na ulisimamia haki.”

Baada ya Zitto kuandika hayo, Polepole aliibuka na kumjibu, “mzee wa kurukia treni kwa mbele ushaanza, mbona unapenda ubashiri na vitendo vya kilozi. Rais hutenda impendezavyo kwa dhamana aliyopewa na Katiba.”

“Sisi tuliohudumu kwenye serikali na chama tunajua na kuheshimu, usijitatafutie huruma kwa mtu acha kupotosha hiyo si siasa safi.”

Katika mabadiliko hayo, nafasi ya Mwigulu imechukuliwa na Kangi Lugola ambaye awali alikuwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Zitto, Polepole wavutana mtandaoni kisa Mwigulu Zitto, Polepole wavutana mtandaoni kisa Mwigulu Reviewed by KUSAGANEWS on July 01, 2018 Rating: 5

No comments: