Wataalam wa afya 6,180 wapangiwa vituo vya kazi


Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imewataka wataalam wa afya 6,180 walioajiriwa kuripoti katika vituo vyao ya kazi ndani ya siku 14

Wataalam hao wa afya watasambazwa katika vituo vya  afya, hospitali za Wilaya na zahanati nchini.

Akizungumza leo Juni 9, 2019 na Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo amesema atakayeshindwa kuripoti ndani ya muda huo, ajira yake atapewa mwingine

Mei 10, 2018 Jafo alitangaza nafasi za ajira hizo na kubainisha kuwa watumishi watakaoajiriwa watapangiwa kwa kuzingatia mahitaji, kuwataka wenye sifa za taaluma katika kada ya afya wajitokeze kuomba nafasi kwa lengo la kutoa huduma kwa wananchi

“Wasijikusanye katika ofisi za mjini kwasababu hatutabadilishia vituo kwa kuwa walipoomba ajira walisema wapo tayari kufanya mahali popote ndani ya Tanzania," amesema Jafo leo

Jafo amesema upangaji wa watumishi hao umezingatia halmashauri ambazo zina zahanati na vituo vya afya lakini hazina watumishi, vituo vya afya 210 ambavyo vilikarabatiwa na zahanati ambazo zilikuwa zinaongozwa na wahudumu wa afya

Ametaka wananchi kuwapokea wahudumu wa afya ili wawatumikie na waache kuwafanyia mambo mabaya kama katika baadhi ya maeneo ilivyokuwa ikifanyika

Amesema majina ya walioajiriwa yanapatikana katika tovuti ya Tamisemi

Wataalam wa afya 6,180 wapangiwa vituo vya kazi Wataalam wa afya 6,180 wapangiwa vituo vya kazi Reviewed by KUSAGANEWS on July 09, 2018 Rating: 5

No comments: