Wananchi Ngorongoro wamkubali Olenasha

Mbunge wa jimbo la Ngorongoro ambaye pia ni naibu waziri wa elimu sayansi na teknolojia William Olenasha akiwa na wananchi wake wa kijiji cha Orkuyene wakati wa alipofanya ziara katika eneo hilo
Wanawake wajasiriamali kijiji cha Erkuyene wakifurahia baada ya kutembelewa na mbunge wa Jimbo la Ngorongoro William Olenasha
Msafara wa wananchi wa kijiji cha Erkuyene tarafa ya Longido  wakiwa wanampokea Mbunge wao alipowatembelea ikiwa ni muendelezo wa ziara yake
Wanafunzi na wananchi waliofika kumsikiliza Mbunge wao aliyefika kijiji cha Erkuyene tarafa ya Longido kwa ajili ya kuwasikiliza wananchi wake


Wananchi wa jimbo la Ngorongoro Mkoani Arusha wamesema kuwa kwa maendeleo ambayo Mbunge wao ambaye pia ni naibu waziri wa elimu ,sayansi na teknolojia Mh William Olenasha ameyaleta hawawezi kubadili mtazamo wa kuchagua Mbunge mwingine kwa miaka ijayo kwasababu amefanya maendeleo ambayo tangu uhuru hayakuwahi kufanyika.

Wameyasema hayo wakati wakizungumza kwenye mkutano wa harambee ya kuchangia vikundi vya wanawake wajasiriamali wadogo wadogo zaidi ya 100 ambapo zilipatikana zaidi ya shilingi Milioni 22 katika kijiji cha Orkuyene tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro.

Katika harambee hiyo ambayo iliendeshwa kwa masaa manne na Mbunge Olenasha ambaye ametoa shilingi Milioni 4 kwa ajili ya akina mama hao zilipatikana zaidi ya shilingi Milioni ishiriki mbili ambazo zitawasaidia wajasiriamali ambao wameamua kujiajiri ili kujipatia kipato.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti mmoja wa akina mama mjasiriamali Kijoa Lepuluka amesema kuwa wamempata mbunge ambaye kama angekuwepo kwa tangu mwanzo wangekuwa na maendeleo zaidi ya walionayo sasa hivi.

“Kweli tunamshukuru sana Mbunge wetu mana ametuletea mabarabara ,Umeme na amejitolea kutusaidia sisi wamama kwakweli tungekuwepo naye tangu nyuma tungekuwa mbali na huyu atakuwa mbunge wetu mpaka atakapoacha mwenyewe” amesema Kijoa Lepuluka

Naye Meseyi Mejoli amesema kuwa Mbunge wao amekuwa akiwapa ushirikano hata anapopigiwa simu anapokea kwa wakati na kama kuna tatizo linapata ufumbuzi kwa wakati.

Kwa upande wa Mejool Maisii amesema kuwa kwa kipindi kirefu wamekosa maendeleo kwasababu viongozi waliopita walikuwa hawajali maslahi ya wananchi wao waliowachagua lakini Mbunge wao wasasa msaada mkubwa.

Amesema kwasasa hawataki siasa chafu ambazo zinaweza kuwarudisha nyuma kimaendeleo na kwamba hawana shida na mbunge mwingine tofauti na olenasha ambaye amewaletea barabara ya Lami,Maji,Umeme na madarasa.

Mbunge Olenasha bado anaendelea na ziara yake ya kutembelea wananchi wa jimbo lake ili kuwaeleza mafanikio aliyoyafanya kama mmbunge na Serikali ya awamu ya Tano inayosimamiwa na Raisi Magufuli.




Wananchi Ngorongoro wamkubali Olenasha Wananchi Ngorongoro wamkubali Olenasha Reviewed by KUSAGANEWS on July 09, 2018 Rating: 5

No comments: