Serikali yaeleza ilivyoshindwa kupata watumishi wenye sifa


Serikali imeshindwa kupata waombaji wenye sifa katika kada za wahandisi vifaa tiba, maofisa wauguzi ngazi ya shahada, wataalam wa mionzi, madaktari wa meno na watalaam wa viungo bandia

Akizungumza leo Jumatatu Juni 9, 2018 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo amewataka wananchi kusomea taaluma hizo kwa kuwa mahitaji ni makubwa mno

“Katika mchakato imebainika kuwapo tatizo la ucheleweshaji wa utoaji wa vyeo vya kitaalam kwa wahudumu katika baadhi ya vyuo na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte)," amesema

Amesema jumla ya waombaji 3,440 wengi wao wakiwa waliomaliza  vyuo mwaka 2016/17 walishindwa kuwasilisha vyeti vya Nacte katika maombi yao ya ajira na kufanya baadhi ya kada kukosa waombaji wenye sifa wa kutosha ikilinganishwa na mahitaji ya Tamisemi

"Ofisi ya Rais Tamisemi imefanya mawasiliano na Nacte ili kuharakisha mchakato wa utoaji vyeti utakaowawezesha wahitimu wote wenye sifa kuweza kuajiriwa," amesema
Serikali yaeleza ilivyoshindwa kupata watumishi wenye sifa Serikali yaeleza ilivyoshindwa kupata watumishi wenye sifa Reviewed by KUSAGANEWS on July 09, 2018 Rating: 5

No comments: