WANAFUNZI wawili wa tumbo moja, Dotto Juma (10), aliyekuwa
anasoma darasa la nne katika shule ya msingi Serengeti wilayani Bunda na Maduhu
Juma (7) aliyekuwa anasoma darasa la awali shuleni hapo, wamekufa maji mtoni
Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Serengeti, Marwa
Samu, watoto hao walikufa maji baada ya kuogelea katika mto mkubwa ulioko
katika eneo hilo na ndipo walipozidiwa na maji na kupoteza maisha
Samo alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 10:00
jioni wakati watoto hao wakiwa wanachunga ng’ombe katika eneo hilo
Kaka mkubwa wa marehemu hao, Kija James, alisema taarifa ya
vifo hivyo ilitolewa na mtoto mwenzao, Kulwa Juma (10) waliyekuwa naye
wakichunga mifugo hiyo
James alisema baada ya kufika katika eneo hilo, walikuta
nguo za watoto hao pembezoni mwa mto na walipomuuliza Kulwa, alisema walikuwa
katika eneo hilo
“Tulifika katika eneo hilo, ambako ni lile lile ulikokutwa
mwili wa tajiri wa mabasi, Super Sammy. Tulipomuuliza Kulwa kwamba wenzake
walikuwa wapi, alitujibu kuwa walikuwa katika eneo hilo,” alisema
“Tulimuuliza kwamba huenda wamekwenda kuchungia ng’ombe
sehemu nyingine akatujibu kwamba walikuwa hapo hapo tu,” aliongeza James
Alisema juhudi za kuopoa miili yao zilifanyika na ndipo
wazamiaji walipoingia ndani ya mto huo na kufanikiwa kuiopoa na kutoa taarifa
polisi
Ofisa mmoja wa polisi wilayani hapa, ambaye hakutaka kutaja
jina lake kwa madai kuwa si msemaji wa polisi, alisema miili ya marehemu hao
ilihifadhiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Bunda na kwamba tayari
imefanyiwa uchunguzi na daktari na kukabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya
mazishi
Wanafunzi wa familia wafa maji wakati wakiogelea
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment