ZAIDI ya abiria 400 wanatarajiwa kusafiri katika safari ya
kwanza ya ndege mpya aina ya Boeing 787-800 Dreamliner kutoka Dar es Salaam-
Mwanza- Kilimanjaro na kurudi Dar es Salaam
Idadi hiyo ya abiria 402 katika safari hizo mbili za
uzinduzi rasmi kesho, za kwenda na kurudi, ambao walikuwa wamekata tiketi hadi
juzi, ni sawa na asilimia 70.8.
Kwa safari moja, ndege hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 284
ambao ni 262 daraja la kawaida na 22 kwa daraja la biashara. Kwa safari mbili
ina uwezo wa kubeba abiria 568 kwa madara hayo mawili
Akizungumzia maandalizi ya mapokezi ya ndege hiyo mkoani
Mwanza juzi, Mkuu wa Mkoa huo, John Mongella, alisema tiketi 244 zimenunuliwa
kwa safari ya saa moja asubuhi na 158 kwa safari ya usiku
“Ninawaomba wananchi wa Mwanza na mkoa jirani fursa kwa
kuwahi kununua tiketi chache zilizobaki," alisema Mongella
Sambamba na wito huo, Mongella aliwataka wananchi wa mkoa
huo na Kanda ya Ziwa kwa ujumla, kutumia fursa ya ujio wa ndege ya Boeing
787-800 kwa maendeleo ya uchumi
Katika ujio huo kwa ndege hiyo kuanza safari za Dar es
Salaam, Mwanza na Kilimanjaro, alisema usafiri wa ndege za Shirika la Ndege la
Tanzania (ATCL) uwe kichocheo cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Alisema serikali imenunua ndege hiyo mpya na ya kisasa kwa
lengo la kuchangia kuinua uchumi wa nchi na kwamba kwenye safari ya kwanza
mkoani hapa, itapokewa rasmi uwanja wa ndege wa Mwanza, saa moja asubuhi
Mkuu wa mkoa aliwaomba wananchi kutoka sehemu mbalimbali za
mkoa wa Mwanza na mikoa jirani kujitokeza kwa wingi kufika uwanjani hapo
kushuhudia mapokezi ya ndege hiyo
Kwa upande wake, Msimamizi wa ATCL Kituo cha Mwanza,
Theonestina Ndyetabula, shirika limejipanga vizuri na linazidi kuimarika, hivyo
kuwaomba wadau wa usafiri wa anga washirikiane kwa kutumia usafiri wa shirika
hilo kupitia ndege zake za "Boeing 787-800 Dreamliner na "Bombadier
Dash 8-Q400
"Matumaini yetu ni kufanya vizuri, kwa kipindi hiki
chote cha ndege hizi hakika tutafanya vizuri. Pia hizo ndege mbili zinafanya
safari katika uwanja wa ndege wa Mwanza mara nne kwa siku," alisema
Ndyetabula
Kuhusu ratiba ya usafiri huo, alisema Mwanza - Dar kupitia
Kilimanjaro ni saa 3:20 hadi 5:40 asubuhi kwa Dreamliner; Mwanza - Bukoba
saa 5:15 hadi 5:45 asubuhi kwa Bombadier
Alisema kwa safari za mchana, Mwanza - Dar ni saa 7:15 hadi
9:00 alasiri mchana kwa Bombadier na usafiri wa usiku Mwanza - Dar ni saa 2:20
hadi 3:40 usiku hiyo kwa Dreamliner
Abiria 400 kukwea Dreamliner safari ya kwanza
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment