MKUTANO wa hadhara wa Mkuu wa Mkoa wa Manyara,
Alexander Mnyeti, umegeuka kaa la moto kwa watumishi wa kujitolea wa
Idara ya Ardhi ya Halmashauri ya Mji wa Babati na wengine kujikuta
vibarua vyao vikiota nyasi
Katika mkutano wake uliofanyika uwanja wa Kwaraa mjini hapa
juzi Mnyeti alidai kukerwa na malalamiko mengi ya wananchi yaliyotawala mkutano
huo kwa asilimia 98
Hali hiyo ilimfanya Mnyeti kumuagiza Mkurugenzi
Mtendaji wa Mji wa Babati, Fortunatus Fwema, kuwatimua
kazi mara moja watumishi wote wa Idara ya Ardhi wanaojitolea ili
wabaki waajiriwa ambao serikali itakuwa rahisi kuwawajibisha
“Watumishi wote wa Ardhi, mkurugenzi waondoe,
siwataki…wabaki waajiriwa na siyo wa kujitolea, maana hawa wote wanaomba rushwa
na ukiona nimefanya hivyo nimefanya utafiti nikabaini wanakula rushwa
“Niliowatuma kufanya upelelezi nao waliombwa
rushwa, mimi wala siogopi kuwaondoa, kabla sijaondolewa mimi
nawaondoa ambao ni ‘saizi’ yangu na kabla sijatumbuliwa ninawatumbua wa
chini yangu,’’ alifoka
Aidha, alimuagiza Katibu Tawala wa Mkoa kumhamisha kazi mara
moja mtumishi mmoja wa ardhi ambaye analalamikiwa na wananchi
Katika hatua nyingine, Mnyeti aliagia
“Mkurugenzi rahisisha masharti ya kupata hati maana upatikanaji wa
hati umekuwa kama vile mtu kwenda Mbinguni, huku wataalam wako
wakijifanya miungu-watu na kuwapoka haki wananchi wanaohitaji hati
zao,’’ alisema
Aidha aliwaonya wataalam wa ardhi wanaowatoza fedha wananchi
na akataka kuambatana na wataalam hao kwenda kuona viwanja vinavyofanyiwa
uthamini akidai kuna harufu ya rushwa
Mnyeti aliwataka wananchi waliochukuliwa ardhi yao lakini
halmashauri imeshindwa kuwalipa fidia kwa muda sasa warudi kwenye ardhi zao
Akizungumzia maamuzi ya Mnyeti, mkazi mmoja wa hapa,
Peter Sulle, alimpongeza kwa hatua alizochukua za kuwaondoa wataalam waliokuwa
wanawaibia watu
Pia alisema agizo la kurudishwa maeneo yao baada ya
halmashauri kushindwa kuwalipa fidia ni uamuzi wa busara
Naye Neema John, alisema, maagizo ya Mnyeti yanapaswa
kutekelezwa kwani baadhai ya watumishi hawawezi kufanya kazi bila kusukumwa
RC Mnyeti ageuka Mbogo Mkutanoni
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 28, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment