NAIBU Waziri wa Viwanda ataka Vipaumbele Vitolewe kwa wahandisi ili Kufikia Tanzania ya Viwanda


NAIBU Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya  ya Juu nchini kutoa kipaumbele kwa Wahandisi na Mafundi Sanifu.

Akizungumza Jijini Arusha  wakati wa kongamano la kwanza la Wahandisi na Mafundi Sanifu katika kuelekea maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa bodi ya Wahandisi, Stella alisema mikopo hiyo itawezesha kuongeza idadi kubwa ya wataalamu hao katika kufanikisha uchumi wa kati wa viwanda.

Alisema mpka sasa takwimu zinaonyesha mafundi sanifu waosailiwa na bodi hiyo ni 927,Wahandisi 22,226 kati yao wanawake ni 2,200 ambayo sawa ni asilimia 10.

"Idadi hii ni ndogo sana ukilinganisha na Rais anavyotamani kuharakisha Tanzaia kuwa na uchumi wa kati wa viwanda hivyo lazima bodi ya mikopp itoe kipaumbele kwa kada hizi muhimu kwa maendeleo yanayokusudiwa,"alisema

Mhandisi Stella alisema serikali inatambua mchango mkubwa wa wataalamu hao katika sekta ya uchumi wa viwanda.
Aidha Stella aliwataka  wataalamu hao kufanya kazi kwa uadilifu na kuzingatia weledi kwani viwanda vingi vya zamani vilikufa sababu ya baadhi ya wataalam kutokuwa waadilifu.

Alisema sekta ya viwanda ni muhimili muhimu katika ukuaji wa uchumi ambapo nchi nyingi zimefanikiwa kupitia viwanda kama China na Vietinam.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Uhandisi Prof.Ninatubu Lema alisema viwanda vingi vinategemea mafundi sanifu na Wahandisi,hivyo hawategemei mwekezaji awekeze kwa kutumia roboti badala ya nguvu kazi.

Alisema changamoto kubwa iliopo katoka sekra hiyo ni uchache wa wataalamu hao na kushauri vema serikali ikawekeza vyuo vikuu,vyuo vya ufundi na shule za Msingi na Sekondari ili kuzalisha wataalamu wengi zaidi.

Kaimu Msajili wa Bodi ya usajili wa Wahandisi, Mhandisi Patrick Barozi alisema kongamano hilo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa bodi hiyo ambapo kilele chake kinatarajia kuadhimishwa Septemba 5 hadi 7 mwaka huu Mkoani Dodoma.

Alisema kongamano hilo litakuwa endelevu na linatarajia kufanyika kila mwaka huku makongamano kama gayo yakifanyika katika mikoa na Kanda mbalimbali nchini.

Aidha alisema uhaba wa wataalamu hao nchini unaathiri utekelezaji wa haraka wa miradi mikubwa kama ya bomba la mafuta.

"Kutokana na uhaba huu Bodi tunatarajia kuleta mafundi Sanifu wa nje ya nchi ili wawafundishe wataalamu wa hapa nchini, kwani tulio nao ni wachache wanakwamisha utekelezaji wa miradi mbalimbali,"alisema
NAIBU Waziri wa Viwanda ataka Vipaumbele Vitolewe kwa wahandisi ili Kufikia Tanzania ya Viwanda NAIBU Waziri wa Viwanda ataka Vipaumbele Vitolewe kwa wahandisi ili Kufikia Tanzania ya Viwanda Reviewed by KUSAGANEWS on July 27, 2018 Rating: 5

No comments: