Chama cha Wanasheria Tanganyika
(TLS) kimesema kitawatumia wabunge wao kupinga muswada wa marekebisho ya Sheria
ya TLS, yaliyowasilishwa bungeni hivi karibuni na Mwanasheria Mkuu wa Serikali
(AG), Dk Aderladus Kilangi
Katika kutekeleza azma hiyo rais wa
TLS, wakili Fatma Karume kupitia barua yake aliyoiandika kwa wanachama wote
akiwaelezea kuwapo kwa muswada huo ametoa wito kwa wanachama kuwatumia wabunge
hao kupinga marekebisho hayo
Fatma katika barua hiyo anasema
muswada huo wa marekebisho ya sheria mbalimbali wa 2018 kifungu cha 108,
kinalielekeza Baraza la Uongozi la TLS lililochaguliwa kuwasiliana na AG kwanza
kabla ya kutengeneza kanuni mpya
Anasema AG ambaye pia ni mwanachama
wa chama hicho, kwake huo ni mfano wa mwanachama mmoja kutumia mamlaka ya Bunge
kujipa haki na mamlaka ndani ya jumuiya ya kidemokrasia
Katika kifungu cha 106(2)(a) cha
muswada huo, wanachama wa TLS ambao si raia wa Tanzania wanazuiliwa kuchaguliwa
katika Baraza la Uongozi. Vilevile katika kifungu cha 106(3) kinawazuia
wanachama ambao ni watumishi wa umma, madiwani, wabunge na viongozi wa vyama
vya siasa kuchaguliwa katika Baraza la Uongozi
Katika kifungu cha 107 cha muswada
huo, wajumbe wa Baraza la Uongozi wanazuiwa kujihusisha na masuala ya kisiasa
Fatma anasema mambo hayo yanayoweka
zuio kwa wanachama wa chama hicho yanayopendekezwa na AG yaliyoingizwa katika
kanuni za uchaguzi za TLS, ambayo sasa yameingizwa bungeni yalikataliwa na TLS
katika mkutano wake mkuu
“Mtizamo wangu wa awali kama rais
wenu ni kwamba marekebisho ya Dk Kilangi ni ya kibaguzi hivyo yanakinzana na
masharti ya Ibara ya 13(1) na 13(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.”
Fatma anasema ataiomba Sekretarieti
ya TLS kuitisha mkutano wa Baraza la Uongozi kujadili hatua za kuchukua kwa
maslahi ya wanachama akiwamo AG.
Akizungumza na gazeti hili kwa simu,
Fatma alisema wana imani wabunge hawatakubali kupitisha sheria hiyo ambayo ni
ya kibaguzi inayokiuka Katiba
Alisema kushiriki masuala ya kisiasa
ni haki yao ya msingi kwa mujibu wa Katiba na kwamba, haiwezi kuchukuliwa na
mtu yeyote.
Akitoa maoni yake kuhusu
marekebisho hayo, wakili Juma Nassoro alisema hana shida na wanachama
kutokujihusisha na masuala ya siasa, lakini tatizo haijafafanuliwa au kutolewa
tafsiri ya wazi ya kujihusisha na siasa
Naye wakili Daimu Halfani alisema
muda na namna ambavyo marekebisho hayo yanafanywa yanaondoa maana halisi,
badala yake picha inayojengeka ni kwamba Serikali inalenga kuwabana wapinzani
ambao ni wanasheria na kuwadhibiti wanasheria kwa ujumla
Halfani alisema tatizo lingine
katika marekebisho hayo ni kutokuwekwa mpaka katika kujihusisha na masuala ya
kisiasa, kufanya shughuli za kisiasa na kutoshirikisha wanachama katika
mapendekezo hayo
Naye wakili Fulgence Massawe alisema kuna
mikataba inayolinda mawakili inataka wawe huru, lakini inavyoonekana Serikali
ni kama inataka kuidhibiti TLS
Wabunge waombwa kupinga marekebisho ya sheria TLS
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 04, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 04, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment