Imeelezwa kuwa kasi ya ongezeko la
Watu Nchini, ni mzigo kwa serikali kwani ndiyo chanzo cha kuibuka kwa
changamoto nyingi katika sekta za jamii, ikiwemo Afya, Elimu na miundombinu.
Hayo yamesemwa na Afisa uhusiano na
mawasiliano, kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu
Duniani (UNFPA), Warren Bright wakati akizungumza amebainisha kuwa kasi
ya ongezeko la watu ni kubwa na haiendani na kasi ya maendeleo ya kijamii na
kupelekea changamoto kuwa kubwa, kwa kuibebesha mzigo mkubwa serikali.
“Matumizi ya uzazi wa mpango imekuwa
ni changamoto kubwa, kuna ongezeko kubwa sana la idadi ya watu na kuna athari
zipo na zitaendelea kuwepo kama jamii haitakubaliana na mabadiliko ya tabia ya
nchi na mazingira Duniani”, amesema
Warren.
Ameongeza kuwa, “ongezeko la
watu Zanzibar kwa sasa limekuwa mara mbili zaidi, hivyo serikali bado
itabebeshwa mzigo tu hata ikitoa huduma za jamii bure, hatuwezi kuhudumiwa
wote”.
Wakati Dunia ikielekea kuadhimisha
siku ya idadi ya watu duniani, Julai 11, Ripoti ya makadirio ya watu nchini
iliyozinduliwa Februari 28, 2018, na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip
Mpango inaonyesha Tanzania kuna idadi ya watu 54.2 milioni hadi kufikia mwaka
2018 huku ikieleza kuwa kila mwaka kuna ongezeko la watu milioni 1.6.
Ongezeko la watu ni mzigo wa serikali
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 03, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 03, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment