Ngorongoro wapata Umeme wa REA tatu


Mbunge wa jimbo la Ngorongoro ambaye pia ni naibu waziri wa elimu sayansi na Teknolojia Mh Wiliam Olenasha amesema mpaka Kufikia mwaka 2019 vijiji 35 vitakuwa vimepata umeme katika mpango wa vijijini REA Awamu ya tatu na baadae wataendelea na maeneo mengine.

Olenasha ameyasema hayo tar 8 August 2018 katika kijiji cha Sakala wakati alipofanya mkutano wa hadhara wa wananchi ambapo amebainisha kuwa kila nyumba lazima itawaka umeme kinachotakiwa ni wananchi kuwa tayari kuupokea umeme huo.

Mbunge Olenasha amesema tayari nguzo za umeme zinaendelea kupita katika maeneo mbalimbali lengo ni kuhakikisha ngorongoro inabadilika kuanzia miundombinu iliyopo mpaka mazingira yenyewe ya maisha ya watu na kuwa ngorongoro mpya.

“Wote ni mashahidi hili hatuzungumzi tena siyo hadithi nguzo tayari zinasambaa katika vijiji tunategemea ifikapo mwaka 2019 vijiji 35 vitakua vinawaka umeme”Alisema Olenasha

Kufuatia ujio huo wa umeme wa REA Mh Olenasha amewataka wananchi sasa kuendelea kujenga nyumba zenye ubora zaidi ili na mazingira yabadilike kwa kuwa Ngorongoro iliyokuwa inajulikana mwanzo kwa migogoro sasa inajulikana kwa maendeleo chanya.

Wakitoa maoni yao baadhi ya wananchi wamesema kuwa ujio wa umeme utawarahisishia sana wao kufanya maendeleo ikiwemo kukuza kipato kwa wafanyabiashara ambao wanategemea umeme tofauti na ilivyo hivi sasa wanapata changamoto ya huduma ya matumizi ya vitu vinavyohitaji umeme.

Katika ziara hiyo ya Mbunge kutembelea wananchi wa jimbo lake wengi wa wadau wa maendeleo pamoja na wananchi wamempongeza Olenasha kwa kuendelea kutekeleza ahadi zake alizoahidi kipindi alipoomba kura ya kuchaguliwa kuwa Mbunge wa jimbo hilo la Ngorongoro.

Jimbo la Ngorongoro lenye kata 28 Olenasha ameshatembelea zote na kuzungumza na wananchi ambapo hii ni mara ya nne kufanya hivyo jambo ambalo wabunge wengi wamekuwa hawafanyi hivyo kufanya muendelea kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wananchi waliowachagua.


Ngorongoro wapata Umeme wa REA tatu Ngorongoro wapata Umeme wa REA tatu Reviewed by KUSAGANEWS on July 08, 2018 Rating: 5

No comments: