Raisi Dkt Magufuli abadilisha historia ya Wilaya ya Ngorongoro iliyokuwa inatambulika kwa Migogoro ya Ardhi
Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro ambaye pia ni naibu waziri
wa Elimu sayansi na Teknolojia Mh William Tate Olenasha amempongeza raisi wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli Kwa kupeleka mradi wa
kihistoria wa ujenzi wa barabara ya lami Kilomita 213 kutoka Loliondo mpaka Mto
wa Mbu ambao Mpaka kukamilika kwake utagarimu kiasi cha Shilingi Bilioni 87.
Olenasha ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na
wananchi wa kata ya Pinyinyi kwenye mkutano wa hadhara katika ziara ya
kuwatembelea wananchi wa jimbo lake ili kuwaeleza mafanikio tangu amechaguliwa
kuwa Mbunge wa Jimbo hilo.
Amesema kuwa mradi huo ni wa kihistoria ambao haujawahi
kutokea tangu kipindi cha kupatikana kwa uhuru na endapo barabara hiyo itakamilika
utarahisisha kukuza uchumi wa wilaya ya Ngorongoro kukua kwa kasi.
Ameongeza kuwa siyo rahisi kupata pesa hizo shilingi
Bilioni 87 kwa kuwa walipita wabunge wengi katika nafasi hiyo lakini serikali
kupitia awamu ya tano ya Raisi Magufuli imebadilisha historia ambayo kwa muda
mrefu baadhi ya watu walijua ni jambo ambalo halitawezekana lakini sasa ujenzi
umeanza.
Mbunge Olenasha amesema kuwa kwa mara ya kwanza
ngorongoro inaingia kwenye ramani ya Tanzania ambapo mradi huo unatekelezwa kwa
vitendo na tayari ujenzi umeshaanza na kwa histori pia hawajawahi kupata
barabara ya Lami licha ya kukaa serikalini kwa muda Mrefu.
Pia ameongeza kuwa lazima amshukuru Mh Raisi kwa niaba
ya wananchi wake kwa sababu haijawahi kutokea kwa kipindi chote cha serikali zilizokua
madarakani.
Olenasha amesisitiza kuwa wilaya ya Ngorongoro ilikuwa
ikitambulika zaidi kwa migogoro ya ardhi lakini kwasasa historia imebadilika
imekuwa wilaya inayokuja kwa kasi katika suala zima la maendeleo
Ameongeza kuwa waandishi wa habari walipokuwa wakija
Ngorongoro walikuwa ni kwa ajili ya kuripoti masuala yanayohusu mvutano wa
ardhi na migogoro lakini kwasasa wanafika kwa picha ya kuwepo kwa maendeleo
kutokana na miradi mikubwa pamoja na kuitangaza ngorongoro ambayo imeandika
historia kwenye ramani ya Nchi ya Tanzania.
Tangu uhuru jimbo la Ngorongoro halikuwahi kuwa hata na
mita moja ya Lami lakini kupitia Mbunge wa Ngorongoro Mh Olenasha kwa
kushirikiana na serikali ya Raisi Magufuli sasa kilomita 213 zinajengwa kwa
lami ambapo historia imeandikwa
Raisi Dkt Magufuli abadilisha historia ya Wilaya ya Ngorongoro iliyokuwa inatambulika kwa Migogoro ya Ardhi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 07, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment