Wilaya ya Ngorongoro imeanza kuandika Historia kwa
upande wa afya baada ya kiasi cha shilingi Bilioni 1 na milioni 500 kutengwa
kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na ujenzi wa vituo 3 vya afya
vya kisasa ambavyo kila kimoja kitagarimu Shilingi Milioni 400.
Hayo yamesemwa na mbunge wa jimbo la Ngorongoro ambaye
pia ni naibu waziri wa elimu sayansi na Teknoloji Mh William Olenasha wakati
akizungumza na wananchi alipokuwa mgeni rasmi wa zahanati ya Neema iliyopo
wilayani Humo.
Olenasha amesema kuwa Ofisi ya Raisi Tamisemi tayari
chini ya Raisi Dokta Magufuli wameshatoa fedha hizo ambapo ujenzi umeshaanza na wananchi wamejitolea eneo kwa
ajili ya Ujenzi ambapo kwa mara ya Kwanza wilaya hiyo inakuwa na Hospitali ya
Serikali ambayo ni ya wilaya.
“Tumeingia kwenye ramani ya nchi kiafya nasisi tutakuwa
na hospitali ya wilaya tunapozungumzia hospitali ya wilaya tunazungumzia kitu
ambacho wote hatuna cha kufananisha nacho katika wilaya yetu kwasababu
haijawahi kuwepo kwahiyo ni tayari ni uwekezaji mkubwa ambao umefanywa na
serikali”Amesema Olenasha
Pia Mbunge Olenasha ameongeza kuwa katika kipindi hicho
cha miaka miwili na nusu cha uongozi wake chini ya Raisi Magufuli wamepata fedha kwa ajili ya ujenzi wa
vituo vitatu vikubwa vya afya kimoja tayari ujenzi kilichoko sakala
kinakamilika cha pili kitajengwa Samunge na kituo cha tatu kitajengwa eneo la
Osinoni ambavyo vyote vitagarimu shilingi Milioni 400.
“Kwa hiyo wanachi wangu kama mkiangalia huo ni uwekezaji
wa zaidi ya shilingi bilioni 3 ndani ya kipindi cha miaka miwili kuna huduma
nyingine zinaendelea na ujenzi unaoendelea wote mnafahamu kwamba katika wilaya
yetu tuna hospitali mbili ile ya enduleni lakini naya Waso ambazo zote ni za
binafsi lakini pia tuna vituo 5 vya afya lakini tuna zahanati 28 ikiwemo hii
hapa kwa hiyo tayari mko tayari kwenye orodha yangu kwenye vituo ambavyo
tunavyo kama mnavyoona tayari tunamaendeleo lakini bado tuna nafasi kubwa ya
kuboresha mazingira ya afya”Amesema Olenasha Mbunge
Pamoja na hayo amewaomba wananchi kujiunga na bima ya
afya kwasababu itakuwa rahisi kila mwananchi kupata huduma kwa bei rahisi zaidi
pamoja na kuborsha huduma za afya.
Kwa upande wa Dokta Richard Nkambi ambaye ni mmiliki wa
zahanati hiyo amesema kuwa kuanzishwa kwa huduma ya afya kutarahisisha utoaji wa huduma ambapo kabla
kituo hicho hakijazinduliwa rasmi kwa mwezi uliopita zaidi ya wananchi 300
wameshapatiwa huduma ambapo matayarijio yao kwa mwezi ni kuhudumia wananchi 600.
“Zahanati hii inaitwa zahanati ya Neema tumejenga kwa
miaka kumi kwa msaada wa NMB kwa kupata mkopo tumandikishwa kisheria kwasasa
tulivyoanza tunatibu kwa mwezi watu 300 lakini tumeweka mikakati kwa
kushirikiana na serikali ili tuboreshe zaidi na kuna vyumba hapa tumetoa bure
kabisa kwa ajili ya huduma ya mama na mtoto.”Amesema Dokta Nkambi
Akizungumza mmoja wa akina mama aliyefika katika kituo
hicho cha afya kupata huduma aliyejitambulisha kwa jina la Mama Mollel amesema
kwa muda mrefua wamekuwa wakipata changamoto lakini baada ya kuwepo kwa kituo
hicho sasa wanajifungua kwa urahisi zaidi kwa kuwa mwanzo walikuwa wanatembea
zaidi ya kilomita 30 kupa huduma ya kujifungua.
Bi Suzan Koila ambaye ni afisa maendeleo ya jamii
mstaafu katika halmashauri ya Ngorongoro amempongeza Mbunge Olenasha kwa
mikakati aliyoieleza mbele ya wananchi kuhusu ujenzi wa hospitali ya Wilaya
pamoja na vituo vya afya ambavyo vitarahisisha zaidi huduma na kufanya afya
iboreshwe.
Magufuli amwaga Mabilioni ya Fedha Ngorongoro Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na vituo vya afya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 07, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment