Rais Magufuli awateua ‘wapinzani’ nafasi za Ukuu wa wilaya


Rais John Magufuli amefanya mabadiliko ya wakuu wa mikoa, wa wilaya na makatibu tawala nchini huku akiwateua wanasiasa watatu waliowahi kuwa vyama vya upinzani katika nafasi hizo

Akitangaza mabadiliko hayo leo Julai 28, Rais Magufuli amemteua David Kafulila kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Songwe

Kafulila aliwahi kuwa mbunge wa NCCR-Mageuzi kabla ya kuhamia CCM

Pia amemteua Moses Machali kuwa Mkuu wa Wilaya ya N
anyumbu. Machali aliwahi mbunge wa Kasulu Mjini, (NCCR-Mageuzi) kabla ya kuhamia ACT-Wazalendo na baadaye CCM

Kadhalika Rais Magufuli amemteua Patrobas Katambi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma. Katambi alikuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema
Rais Magufuli awateua ‘wapinzani’ nafasi za Ukuu wa wilaya Rais Magufuli awateua ‘wapinzani’ nafasi za Ukuu wa wilaya Reviewed by KUSAGANEWS on July 28, 2018 Rating: 5

No comments: