Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Ngenya Athuman
Yusuf kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu
Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. Ngenya Athuman Yusuf
umeanza tarehe 30 Juni, 2018.
Kabla ya uteuzi huo Dkt. Ngenya
Athuman Yusuf alikuwa Mhadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Waislamu cha
Morogoro (MUM).
Dkt. Ngenya Athuman Yusuf amechukua
nafasi ya Prof. Egid Beatus Mubofu ambaye ameteuliwa kuwa Makamu Mkuu wa Chuo
Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Rais Magufuli afanya uteuzi mwingine
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 03, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 03, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment