Serikali imezindua mkakati wa kupambana na biashara haramu
ya binadamu, huku Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola akisema watapita
nyumba kwa nyumba kubaini wanaotumikishwa wakiwamo wasichana wa kazi za ndani
Kwa mujibu wa Umoja wa Mtaifa, Tanzania ni miongoni mwa nchi
zenye tatizo la usafirishaji wa binadamu.
Akizungumza katika
maadhimisho ya siku ya kupinga biashara haramu ya usafirishaji binadamu, Lugola
alisema si rahisi kufikia maendeleo yanayotajwa ikiwa biashara hiyo ndani ya
nchi itaachwa. “Hatuwezi kuendelea kuwa na kundi la watu linalojihusisha na
usafirishaji wa binadamu, hii ni sawa na utumwa,” alisema
Alisema watu wengi wakiwamo watoto wanaotumbukia kwenye
biashara hiyo hudanganywa kupewa kazi lakini wakifika maeneo husika, hukutana
na kazi nje ya makubaliano yao
Lugola alisema wapo waajiri wanaotumia nguvu ya fedha na
sheria za kazi kama kichaka cha kuwatumikisha wengine ambao wakibainika
watashughulikiwa
Kuhusu biashara haramu ya binadamu kwa Watanzania
wanaotumikishwa nje ya nchi, Lugola alisema wengi wao hudanganywa kwa mishahara
mikubwa na kazi zenye staha tofauti na hali wanayoikuta huko.</p></div><div><p>Alisema
zaidi ya Watanzania 22, nje ya nchi wamejisalimisha kwa kutoa taarifa za
kutumikishwa
Naye mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti Biashara Haramu ya
Usafirishaji Binadamu, Abeatus Magere alisema kati ya mwaka 2015 na 2018 watu
327 wameokolewa kutoka biashara hiyo
Alisema kati yao, watu 45 ni wageni kutoka nje ya nchi
“Tangu mwaka 2015 hadi mwaka huu kesi 24 zimefikishwa
mahakamani na saba kati yake, wamepatikana na hatia,” alieleza
Magere alisema uzoefu wao unaonyesha kuwa vita hiyo ni ngumu
na inaweza kuhatarisha maisha kwa wale wanaopambana kuidhibiti
Mratibu wa mradi kutoka Shirika la Utetezi wa Haki za Watoto
na Wanawake (Kiwohede), Eda Kawala alisema Serikali haina budi kufanya
uchunguzi wa kina kujua ukubwa wa tatizo la usafirishaji wa binadamu nje ya
nchi
Alisema kituo chao kwa sasa kina watoto wawili wa biashara
hiyo ndani ya nchi na wengine kumi waliofanyiwa ukatili mbalimbali
Kawala alisema mwaka jana walimuokoa mtoto wa miaka 13
aliyekuwa anatumikishwa japo alipopimwa alikuwa mjamzito na tayari alikuwa
ameambukiwa magonjwa ya zinaa vikiwemo virusi vya Ukimwi
Alishauri Serikali kuandaa sheria itakayowabana
wasafirishaji na wale wanaofanikisha mpango wa biashara hiyo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 30, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment