Wakati mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya HaliHalisi, Saed
Kubenea amesema Jumatano ijayo atachapisha nakala ya kwanza ya gazeti la
Mwanahalisi baada ya kushinda kesi katika Mahakama Kuu, Serikali imesema haina
taarifa na ujio huo
Kubenea aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba, gazeti
hilo limeshinda kesi iliyofunguliwa mwaka 2017 katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar
es Salaam na uamuzi umefanyika hukumu ilitolewa Jumanne ya wiki iliyopita
“Kama kampuni Jumatano ya wiki ijayo, tutachapisha nakala ya
gazeti hilo kwa mara ya kwanza tangu lifungiwe,” alisema
Alisema taratibu za kuomba leseni zinaendelea lakini gazeti
kwa mujibu wa sheria halihitaji kusajiliwa tena badala yake, Mahakama imeamuru
lifunguliwe na liendelee kuchapishwa
Kubenea ambaye pia ni mbunge wa Ubungo (Chadema), alisema
Mahakama imesema mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) hana mamlaka yoyote
siyo tu kuomba watoe maelezo ni kwa nini walichapisha habari hiyo, bali hata
kuwaomba wapeleke utetezi wao
Hata hivyo, mkurugenzi wa Maelezo ambaye pia ni msemaji wa
Serikali, Dk Hassan Abbas alisema wao kama Serikali hawana taarifa ya hukumu
hiyo
“Unayo nakala ya hukumu hiyo? Sisi hatuna kama ameshinda au
hajashinda sina taarifa zake,” alisema
Alisema mbali na kutokuwa na taarifa ya kushinda kesi hiyo,
kuna taratibu chini ya sheria ya huduma za habari zinazotakiwa kufuatwa kabla
gazeti halijachapishwa. “Sheria hiyo imeanza kutumika Desemba 31 mwaka 2016
ambayo inaeleza kwa namna yoyote ile hakuna gazeti litakaloruhusiwa kuchapishwa
bila kuwa na leseni period (basi), ”alisema Dk Abbas
Kubenea alisema wananchi waendelee kuuamini mhimili wa
mahakama, wasiache kudai haki zao mahakamani, kuweka mawakili wazuri na
kuwasilisha ushahidi usio na shaka kwa sababu mahakama zipo huru
Awali, mwanasheria wa kampuni hiyo, Nashon Nkungu alisema
Mahakama imesema amri ya kulifungia gazeti hilo ni batili na haikufuata
taratibu za sheria ikiwamo kutokuwa na haki ya usikilizwaji kwa upande wa
mlalamikaji
Pia, alisema Mahakama ilieleza kuwa mkurugenzi wa maelezo
hakuwa na mamlaka ya kutoa amri hiyo wala kuchukua uamuzi hayo
Serikali yasema haina taarifa ujio wa Mwanahalisi mtaani
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 30, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 30, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment