"Nilipochaguliwa na wananchi wa Ngorongoro Niliahidi Maji,Barabara,Afya na Elimu wenyewe Mnaona "Mbunge Olenasha
Mbunge wa jimbo la Ngorongoro amesema maendeleo ambayo
yanakuja kwa kasi pamoja na miradi mikubwa ya maendeleo ni kwasababu ya
ushirikiano wake na wananchi waliomchagua kuwawakilisha Bungeni.
Akizungumza katika ziara yake ya Jimbo kutembelea
wananchi wake na kuwaeleza mafanikio yaliopatikana kwa miaka miwili tangu
alipochaguliwa na wananchi wake Olenasha amesema wananchi wamekuwa mstari
wa mbele katika kuleta maendeleo ambayo kwasasa yanaonekana
Olenasha amesema alipochaguliwa na wananchi aliapa kuhakikisha
maendeleo ya maji,barabara ya lami,Afya,Umeme pamoja na elimu bora yanaenda kwa
wananchi waliompigia kura awe muwakilishi wao kitu ambacho ametekeleza na sasa
miradi inaendelea kujengwa.
Amesema yeye kama Mbunge hapendi kuona wananchi wake
wanateseka wakati yeye yupo na anauwezo wa kutekeleza aliyoyaahidi siku ambapo
alisimama jukwaani kunadi sera ambazo zimempa yeye kuwa mbunge.
“Wananchi wangu mimi mmenichagua nisumbueni nitumeni
ndiyo mana nimerudi kwenu mimi siyo Mbunge wa kupotea potea na mpaka sasa hivi
nyie wananchi wangu ni mashahidi tangu nimekuwa muwakilishi wenu nimepita kila
kata mara nne na sasa nimerudi tena na nitaendelea kuja na sitawachoka”Alisema
Olenasha
Olenasha ameongeza kuwa kila akitembea anawaza maendeleo
ya wananchi wake waliomchagua ambao wamempa mzigo wa kuwatumikia chini ya
serikali ya Awamu ya Tano ya Raisi Dokta John Pombe Magufuli ya hapa Kazi tu.
Hata hivyo amesema yuko tayari kurudi katika jimbo lake mara kwa mara kwa ajili ya wananchi licha ya kuwa na majukumu mengi ya kiserikali atarudi kila wakti kwa ajili ya kushirikiana na wananchi kusimamia miradi mikubwa ya maendeleo iliyopo
Akizungumza mmoja wa mwanachi katika kata ya Samunge
Bwana Modeli Kibwana amesema kuwa kwasasa mbunge waliyempata amewaletea
maendeleo kuliko kipindi chochote kile cha viongozi waliopita
Amesema Mbunge Olenasha amekuwa mstari wa mbele
kusimamia miradi anayoileta na wanaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa
kushirikiana na Mbunge wao kufanya mambo yaliyoshangaza kila mtu aliyekua
anaijua Ngorongoro kwa migogoro.
Naye Jumanne Bwanga amesema kwamba hawatarajii kuona mtu
anawatoa kwenye mstari wa maendeleo na wao kama wananchi watahakikisha miradi
inayoletwa kupitia Mbunge wao wataisimamia kwa nguvu zote bila kuhujumiwa.
"Nilipochaguliwa na wananchi wa Ngorongoro Niliahidi Maji,Barabara,Afya na Elimu wenyewe Mnaona "Mbunge Olenasha
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 11, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment