Ndugai atoa neno kujizulu Waitara

Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema amepokea barua kutoka kwa aliyekuwa mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara ya kujivua uanachama wa Chadema na kujiuzulu wadhifa huo

Ndugai amesema hayo leo Jumatatu, Julai 30 akiwa Ikulu jijini hapa wakati wa hafla ya Rais John Magufuli kutoa hati za viwanja vilivyopo Dodoma kwa mabalozi 62 wa nchi mbalimbali na mashirika matano ya kimataifa kwa ajili ya kujenga ofisi na makazi

“Kwa kuwa nimeambiwa ninaonekana nchi nzima, napenda nitangaze kuwa leo asubuhi nimepokea barua kutoka kwa mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara kuwa amejivua 
uanachama wa chama chake na kujiuzulu ubunge’ amesema Ndugai ambaye alikaribishwa kutoa salamu kutoka Dodoma
Ameongeza ataiandikia barua Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ili taratibu zifuate

“Kilichobakia ni kuiandikia Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa rasmi jimbo la Ukonga liko wazi’ ameseam Ndugai
Waitara alitangaza kujivua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM Jumamosi iliyopita.

Ndugai atoa neno kujizulu Waitara Ndugai atoa neno kujizulu Waitara Reviewed by KUSAGANEWS on July 30, 2018 Rating: 5

No comments: