Mbowe asema Chadema haitishiki na wanaotimkia CCM


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amewataka viongozi, wanachama, wafuasi na wapenzi wa chama hicho kutotishika na wimbi la viongozi na wanachama wanaohamia vyama vingine akisema linakipa chama hicho fursa ya kujiimarisha

“Wale wanaokimbilia vyama vingine wanakiimarisha zaidi chama chetu kwa sababu kinatupa fursa ya kubaki na viongozi na wanachama wenye uchungu na nia ya dhati ya kukijenga chama chao,” alisema Mbowe

Akihutubia mkutano wa kampeni kumnadi mgombea udiwani katika uchaguzi mdogo kata ya Turwa wilayani Tarime jana Julai 29, 2018 Mbowe alisema Chadema iko imara kulinganisha na wakati mwingine kutokana na kubakiwa na watu wenye nia ya dhati ya kukipigania

“Wanaofika bei kwa ahadi ya fedha au vyeo waondoke mapema na ninawahakikishia Chadema itaendelea kuwa taasisi imara zaidi kuliko ilivyo sasa,” alisema Mbowe

Bila kutaja majina, kiongozi huyo alisema chama hicho kimewahi kuondokewa na viongozi wa ngazi za juu kiasi cha wengi kudhani kingeyumba lakini ikawa kinyume chake kwa kuimarika na kupata wabunge, madiwani na wachama wengi zaidi

Viongozi wa kitaifa waliowahi kujiondoa Chadema ni aliyekuwa Katibu Mkuu, Dk Wilbrod Slaa na Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa zamani Dk Amani Walid-Kaborou
Mbowe asema Chadema haitishiki na wanaotimkia CCM Mbowe asema Chadema haitishiki na wanaotimkia CCM Reviewed by KUSAGANEWS on July 30, 2018 Rating: 5

No comments: