Jalada kesi ya vigogo wa madini lipo kwa DPP


Jalada la kesi ya uhujumu uchumi, inayomkabili Mkurugenzi wa Uthaminishaji Madini ya Almasi na Vito Tanzania, Archard Kalugendo na mwenzake, bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini( DPP) kwa ajili ya uamuzi

Mbali na Kalugendo, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Mthamini Almasi wa Serikali, Edward Rweyemamu ambao ni waajiriwa wa Wizara ya Madini

Wakili wa Serikali, Halid Nasua amedai leo JUlai 30, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Hamis Ally, wakati kesi hiyo ilipotajwa

Nasua amedai kesi ilikuja kwa ajili ya kutajwa, upeĺelezi bado haujakamilika na kwamba jalada la shauri hilo lipo kwa DPP kwa ajili ya kulipitia na kulifanyia uamuzi

Baada ya kueleza hayo aliomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la

Hata hivyo, wakati upande wa mashtaka wakiomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa, upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Ludovick Nickson na Kabula Swedish uliutaka upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi wao kwa wakati, kwa sababu wateja wao wanaendelea kusota mahabusu

Hakimu Ally, baada ya kusikiliza hoja hizo aliiahirisha kesi hiyo hadi Julai 30, 2018 kwa ajili ya kutajwa

Kalugendo na Rweyemamu wanasota mahabusu kutokana na DPP kuzuia dhamana zao na wanakabiliwa na  kesi ya uhujumu uchumi wakidaiwa kuisababishia Serikali hasara ya Sh2.4 bilioni
Katika hati ya mashtaka, washtakiwa wanakabilkiwa na shtaka la kuisababishia Serikali hasara ya Sh2.48 bilioni ambapo wanadaiwa kutenda kosa hilo kati ya Agosti 25 na 31, 2017 katika maeneo mbalimbali ya mikoa ya Dar es Salaam na Shinyanga

Washtakiwa hao wanadaiwa  kwa pamoja na kwa vitendo vyao wakiwa wathaminishaji wa almasi wa serikali na waajiriwa wa wizara hiyo waliisababishia serikali hasara ya Dola za Marekani 1,118,291.43  ambazo ni sawa na Sh2.48 bilioni
Jalada kesi ya vigogo wa madini lipo kwa DPP Jalada kesi ya vigogo wa madini lipo kwa DPP Reviewed by KUSAGANEWS on July 30, 2018 Rating: 5

No comments: